Nyota wapya yanga wajifua na kikosi cha yanga

Uongozi wa Yanga tayari umewapokea nyota wanne wa kigeni wanaotarajiwa kusajiliwa na timu hiyo kwa ajili ya msimu ujao

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema anatarajia kukamilisha usajili wa nyota sita wa kigeni pamoja na wazawa wawili kabla ya kuondoka kwenda DR Congo kujiunga na kambi ya timu ya Taifa

Nyota wa kigeni waliohudhuria mazoezi ya Yanga jana ni pamoja na kiungo mwenye umri wa miaka 20 raia wa Nigeria Victor Patrick Akpan aliyekuwa akikipiga na JKU ya Zanzibar

Akpan yuko kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Nigeria umri chini ya miaka 23

Wengine ni beki wa kati Mohammed Ali Camara mwenye umri wa miaka 21 kutoka klabu ya Horoya AC ya Guinea.

Camara aliitumikia timu ya Taifa ya Guinea U20 na tayari ameitumikia timu ya wakubwa mara moja

Wengine ni mshambuliaji Shehu Magaji Bulama raia wa Nigeria na kiungo Allex Komenan kutoka nchini Ivory Coast

Bulama na Komenan watafanyiwa majaribio na Zahera kabla kuidhinisha kama wasajiliwe au la

Sherehe za Ubingwa Simba Kufanyika Leo

Mabingwa wa nchi Simba leo wanakabidhiwa taji la pili mfululizo ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya mchezo dhidi ya Biashara United

Mchezo huo utaanza mapema tu, saa tisa Alasiri ambapo hafla ya makabidhiano ya ubingwa itafanyika baada ya mchezo huo

Waziri wa Mambo ya Ndani Mh Kangi Lugola anatarajiwa kuwa mgeni wa rasmi katika hafla hiyo itakayofanyika uwanja wa Taifa

Uongozi wa Simba umewataka mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanja wa Taifa leo kushuhudia tukio hilo litakalobaki kwenye kumbukumbu za klabu ya Simba

Hilo ni taji la 20 la ligi kuu ya Tanzania Bara kwa Simba

Baada ya kuichachafya Sevilla juzi, Aussems amepania kushusha mziki kamili ili kunogesha sherehe za ubingwa kwa ushindi mnono

Viingilio vya mchezo huo, VIP A Tsh 15,000/- VIP B na C Tsh 10,000/- wakati mzunguuko ni Tsh 3,000/-

Kocha wa Sevilla Amvulia Kofia John Bocco, Adai Ana Kiwango Kama cha Drogba

Mkufunzi wa sevia kutoka laliga ya Spain ameshangazwa na uwezo wa john boco drogba kwa kysema hakudhania Kama Tanzania kuna vipaja namna hii!!

Alisema namnukuu “I have never been in east Africa especially Tanzania, I used to know some talented from Africa like drogba and keita but to me that young man with number 22 kit is really magnetic, classical and professional”

Reporter: would you ever sign him?

Why not’ any manager would like to work with “booock’o (Spanish articulation) but i know it is not easy to sign a player from simba which is the richest club in central and east africa

Reporter, three players from simba with best performance tonight boco excluded?

I think kaaagere, nyoni and mkuude performed well

Huyu boco hatari sana tusishangae kesho akalambishwa mkataba na sevia’

Kila la kheri boko umri unaruhusu Wewe bado kijana mdogo na haujapunguza umri

MKUDE Haendi Popote – MO

Mwenyekiti wa Bodi wa Wakurugenzi ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ amewatoa hofu wapenzi, wanachama na mashabiki wa timu hiyo juu ya kiungo mkata umeme Jonas Mkude

Mo amesema Mkude ataendelea kubaki Msimbazi

Mkude amekuwa akihusishwa na timu kadhaa ikiwemo klabu ya Yanga inayodaiwa kumuahidi zaidi ya Tsh Milioni 120

Wanasimba msiwe na wasiwasi, Mkude haendi popote! Jumaah Kareem,” ameandika Mo kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram

Mkude ni miongoni mwa wachezaji waliomaliza mikataba Simba na alikuwa akisubiri kusaini mkataba mpya wa kuendelea kubaki Msimbazi

SIMBA vs BIASHARA UNITED TAIFA

Mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Biashara United utakaopigwa kesho Jumamosi, May 25, umehamishiwa uwanja wa Taifa na utaanza saa tisa Alasiri

Mabadiliko hayo yatatoa nafasi kwa Simba kukabidhiwa ubingwa baada mchezo huo kumalizika

Uongozi wa Simba umethibitisha mabadiliko hayo na kuwataka mashabiki wa timu hiyo wajitokeze kwa wingi kesho uwanja wa Taifa kupokea ubingwa wa ligi kuu

“Mchezo wa Ligi Kuu ambao tutacheza kesho dhidi ya Biashara United utachezwa katika Uwanja wa Taifa kuanzia saa 9:00 alasiri. Sababu ya mabadiliko ya muda ni sherehe za kukabidhiwa kombe la ubingwa wa Ligi Kuu 2018/2019 ambazo zitafanyika baada ya mechi kuisha,” imesema taarifa ya Simba

TEN: Awaaga AJIBU, MAKAMBO: Amkaribisha KOUKPO

Heritrier Makambo na Ibrahim Ajib wamebakisha wiki moja tu ya kuitumikia Yanga kwani baada ya mchezo dhidi ya Azam Fc, wachezaji hao hawatakuwa mali ya Yanga

Wakati Makambo akisubiri kutimkia Horoya AC, Ajib anaelekea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kujiunga na mabingwa wa nchi hiyo, TP Mazembe

Afisa Habari wa Yanga Dismas amewatakia kila la kheri wachezaji hao waliokuwa na mchango mkubwa kwa kikosi cha Yanga msimu huu

Wakati Makambo akifunga mabao 17, Ajib amehusika katika mabao 23, akitengeneza 17 na kufunga sita

Ten amesema wawili hao wangetengeneza ‘combination’ ya hatari na Marcellin Koukpo ambaye anatajwa kusajiliwa na Yanga

“Simba kuna utatu wa Kagere, Bocco na Okwi nawaza sijui ingekuwaje kama nasi tungepata utatu wa Ajib, Makambo na Koukpo”

“Simaanishi kwamba waliokuwepo hawawezi, lakini wakati mwingine si vibaya kuwaza kwa mafanikio ya mwingine. Kikubwa kila timu ijenge kikosi imara ili tuwe na ligi ya ushindani kweli mwakani” amendika Ten kwenye ukurasa wake wa Instagram

Yanga itamkumbuka Ajib kwa mchango wake aliotoa kwa klabu hiyo tangu alipojiunga kutoka Simba misimu miwili iliyopita, wakati Makambo amecheza Yanga kwa msimu mmoja lakini atakumbukwa kwa uhodari wake wa ‘kuzijaza’ mabao timu pinzani

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera ana kazi ya kusaka wachezaji watakaoziba nafasi zao.

Mwenyewe amewatoa hofu mashabiki wa Yanga akiwahakikishia kuwa atasajili wachezaji wenye uwezo sawa au zaidi yao

Majembe ya nje yanayoshuka yanga ni ya KIMATAIFA

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema wachezaji wa kigeni wanaotarajiwa kusajiliwa na timu hiyo wote wanacheza katika timu zao za Taifa

Zahera amesema usajili wa wachezaji wa kigeni umezingatia umuhimu wa kusajili wachezaji ambao wataongeza ushindani na kuinua kiwango cha wachezaji wa ndani

“Miongoni mwa wachezaji tutakaowasajili, sita au saba ni wachezaji wa kigeni. Wageni wote wanaokuja Yanga wanacheza timu za Taifa. Watasaidia kuongeza ushindani wa kikosi chetu na kuinua viwango vya wachezaji wazawa,” amesema

Kuhusu usajili wa wachezaji wa ndani, Zahera amesema hawatafanya usajili mkubwa wa wachezaji wa ndani

“Nafikiri tutasajili wachezaji watatu au wanne wa ndani. Tunao wachezaji wazuri ambao tutawaimarisha ili msimu ujao wawe bora zaidi”

Kuhusu wachezaji wanaoachwa, Zahera amesema wataachana na wachezaji 10 ambao majina yao yatafahamika baada ya kumalizika kwa mchezo wa mwisho wa ligi dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa Jumanne, May 28 2019