SIMBA Yamalizana na Bocco

Klabu ya Simba inaendelea na mchakato wa kuhuisha mikataba ya wachezaji wake ambayo inamlizika na tayari imemalizana na nahodha wake John Bocco

Taarifa za uhakika ni kwamba Bocco amesaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kukipiga Msimbazi hadi mwaka 2021

Bocco aliyeifungia Simba mabao 15 kwenye ligi ya Tanzania Bara msimu huu, alikuwa akiwaniwa na timu yake ya zamani Azam FC

Azam Fc inadaiwa kuwashawishi Aishi Manula, Erasto Nyoni, John Bocco na Shomaria Kapombe wasaini kunako klabu hiyo waliyokuwa wakicheza kabla ya kusajiliwa na Simba mwaka juzi

Msimu uliopita Bocco aliibuka kuwa mchezaji bora wa Simba na msimu huu ameteuliwa kuwania tuzo hiyo sambamba na Meddie Kagere na Clatous Chama

Zoezi la kuchagua mchezaji bora wa msimu huu tayari limeanza, kura zinapigwa kupitia tovuti rasmi ya Mo Simba Awards

Bonyeza HAPA kumpigia kura Bocco kama unadhani anastahili kuwa mchezaji bora wa Simba msimu huu

CAF Yatangaza Gharama za Tiketi Nchini Misri

Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) limetangaza gharama za tiketi za kutazama mechi za Fainali za Africa (AFCON) zinazotarajia kuanza mwezi ujao nchini Misri.

Kwa upande wa Shrikisho la soka nchini TFF limethibitisha taarifa hiyo, ikisema kuwa CAF imetangaza gharama hizo kwa madaraja mbalimbali, kwenye michezo ya hatua ya makundi ambayo itahusisha timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) tiketi za daraja la kwanza ni USD 29 ambayo ni sawa na takribani sh 66,700 za Kitanzania, tiketi za daraja la pili ni USD 18 ambazo ni sawa na sh 41,403 tiketi za daraja la tatu ni USD 6.

Katika hatua ya makundi, Taifa Stars itacheza michezo mitatu ambapo itaanza dhidi ya Senegal ikifuatiwa na mchezo dhidi ya Kenya na kumalizia hatua hiyo kwa kucheza na Algeria

Aidha, Kwenye hatua ya robo fainali gharama ya tiketi daraja la kwanza ni USD 35 ambayo ni takribani sh 80,521 kwa daraja la pili ni USD 24 na daraja la tatu ni USD 12.

Hatua ya nusu fainali, tiketi daraja la kwanza ni USD 59 ambazo ni sawa na sh 135,700, daraja la pili ikiwa ni USD 29 na daraja la 3 USD 18. Mchezo wa mshindi wa 3 utakua na gharama ya USD 35 kwa daraja la kwanza, USD 24 kwa daraja la 2 na USD 12 daraja la 3.

Mchezo wa fainali, daraja la kwanza ni USD 106 ambazo ni takribani sh 243,800, daraja la 2 ni USD 44 ambazo ni takribani sh 101,200 na daraja la tatu ni USD 24.

Pia TFF imesema kwa yoyote mwenye nia ya kununua tiketi hizo za AFCON awasiliane na shirikisho hilo mapema kabla ya kufungwa kwa muda wa maombi.

MAKAMBO Ajaza Pesa JANGWANI

Yanga imefikia makubaliano na klabu ya Horoya Fc kumuuza mshambuliaji wake Heritier Makambo aliyesaini kunako klabu hiyo mkataba wa miaka mitatu

Habari njema ni kuwa Yanga itafanya biashara ya faida kwani itaingiza zaidi ya Mil 230, ikipata faida ya zaidi ya Mil 170

Makambo alitua Yanga akitokea klabu ya FC Lupopo ya DR Congo kwa dau la takribani Milioni 60

Yanga inaendelea na mchakato wa kukiboresha kikosi chake na bila shaka fedha hizo zitatumia katika usajili unaoendelea

Makambo tayari ametambulishwa kunako klabu ya Horoya Fc, mabingwa wa Guinea

Mkurugenzi wa Ufundi wa Horoya Jaid Martin wiki ijayo atakuwa jijini Dar es Salaam kumalizana na Yanga ili kukamilisha taratibu za mwisho za usajili wa Makambo

Uongozi wa Yanga kupitia Mwenyekiti Dk Mshindo Msolla amethibitisha kuwa na taarifa ya Makambo kwenda kufanyiwa vipimo vya afya

“Ni kweli Makambo aliondoka juzi na mwalimu Zahera kuelekea Guinea kwa ajili ya vipimo kwa klabu ya Horoya huko Guinea,” amesema Dk Msolla

“Tunasubiri warudi tuitazame ofa yao kisha tufanye biashara. Taarifa za kutambulishwa rasmi sizielewi ila mwalimu akirudi tutaitazama ofa yao kulinganisha na klabu zingine nyingi zinazomtaka kisha tutafanya maamuzi”

ZAHERA : Asaka Mrithi wa MAKAMBO

Baada ya kusambaa kwa taarifa za mshambuliaji wa Yanga Heritier Makambo kusajiliwa na Horoya AC ya Guinea kwa mkataba wa miaka mitatu, Mwenyekiti wa Yanga Dk Mshindo Msolla alifafanua kuwa dili hilo limeihusisha klabu yake na Makambo aliondoka nchini na Kocha Mwinyi Zahera

Hata hivyo imefahamika Zahera alilekea nchini Bennin ambako amekwenda kufanya mazungumzo na mshambuliaji mwingine

Halitakuwa jambo la kushangaza kama mshambuliaji huyo atakuwa Marcellin Koukpo ambaye alikuja msimu uliopita lakini usajili wake kukwamishwa na wajanja wachache waliokuwa wakitaka ‘ten percent’

Koukpo mshambuliaji wa Kimataifa wa Benin, alikaa nchini kwa zaidi ya wiki mbili kabla ya kuamua kuondoka baada ya kupishana na viongozi wa Yanga

Mshambuliaji huyo alipendekezwa na aliyekuwa kocha wa Yanga msimu uliopita, George Lwandamina na alifanyiwa majaribio na kocha Mwinyi Zahera kabla ya kuibuliwa taarifa za ‘uzushi’ kuwa ameshindwa majaribio

Baada ya kumuuza Makambo, Yanga inaweza kusajili washambuliaji wawili ambapo mmoja anaweza kuwa huyo Mbenin huku timu hiyo ikihusishwa na mshambuliaji wa Gor Mahia Jacques Tuyisenge na Roderick Matuma raia wa Zimbabwe anayekipiga kunako klabu ya Fc Lupopo

Dirisha la usajili litafunguliwa mwezi ujao ambapo uongozi wa Yanga umepania kukiimarisha kikosi chake wakijipanga kutumia kati ya Bil 1.5 hadi Bil 2

Hata hivyo Yanga imedhamiria kukamilisha masuala ya usajili mapema hasa ikizingatiwa Zahera ndiye msimamizi Mkuu wa mchakato huo

Mwanzoni mwa mwezi wa sita Zahera atarejea kwao Congo kwa ajili ya majukumu ya timu ya Taifa kuelekea fainali za AFCON zitakazofanyika Misri kuanzia Juni 21 2019

SIMBA inamkumbuka Patrick Mafisango

Tarehe kama ya leo miaka saba iliyopita, May 17 2012 klabu ya Simba ilipatwa na majonzi makubwa baada ya kumpoteza kiungo wake Patrick Mafisango aliyefariki kwa ajali ya gari

Umauti ulimfika Mafisango kupitia ajali ambayo katika jitihada za kunusuru maisha ya mwendesha pikipiki, gari yake iliingia mtaroni na kusababisha apoteze maisha kutokana na majeraha aliyopata

Kabla ya kuja Tanzania Mafisango alichezea APR ya Rwanda na alipofika nchini alijiunga na Azam Fc kabla ya kusajiliwa na Simba

Mechi ya mwisho Mafisango kuichezea Simba ilikuwa dhidi ya Al Ahly Shandy nchini Sudan katika hatua ya 16 Bora ya Kombe la Shirikisho, ambayo Simba ilitolewa kwa penalti 9-8, kufuatia sare ya jumla ya 3-3.

Hadi anafariki dunia, Mafisango alikuwa ni tegemeo Simba katika safu ya kiungo

Pamoja na kucheza kama kiungo, Mafisango pia anamudu kucheza nafasi ya beki wa kushoto na beki wa kati

KRC GENK anayochezea mtanzania Mbwana Samatta imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi kuu nchini Ubelgiji

Klabu ya KRC GENK anayochezea mtanzania Mbwana Samatta imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi kuu nchini Ubelgiji maarufu kama Belgium Pro League mara baada ya kutoka sare ya 1-1 dhidi ya Anderlecht huku ikisaliwa na mchezo mmoja mkononi.
.
Genk itamaliza mchezo wake wa mwisho ikiwa nyumbani dhidi ya St.Liege.
.
.
Hongera @samagoal77

BREAKING NEWS: MAKAMBO ATIMKA YANGA, AJIUNGA HOROYA AC

Mshambuliaji wa Yanga Heritier Makambo ametimkia Guinea kujiunga na klabu ya Horoya Fc

Taarifa za Makambo kusajiliwa na Horoya zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii mapema leo ambapo timu hiyo imemtambulisha rasmi
Makambo ndiye kinara wa mabao katika kikosi cha Yanga msimu huu akitupia kambani mabao 16

Kulingana na mtandao wa Kalonews, Makambo amesaini mkataba wa miaka mitatu

“Horoya AC imemsajili mshambuliaji kutoka DR Congo Heritier Makambo aliyekuwa akiichezea Young Africans ya Tanzania,” imesema taarifa ya mtandao huo

“Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 25 aliyewahi kuichezea Motema Pembe, amefunga mabao 16 kwenye ligi ya Tanzania”
“Amesaini mkataba wa miaka mitatu”

Kuondoka kwa mshambuliaji huyo ni pigo kwa Yanga ambayo iko kwenye mchakato wa kukiimarisha kikosi chake kwa ajili ya msimu ujao

https://play.app.goo.gl/?link=https://play.google.com/store/apps/details?id=com.chumbani.raha&ddl=1&pcampaignid=web_ddl_1

Yanga italazimika kuingia sokoni kusaka washambuliaji wengine wakali

Hata hivyo Yanga itanufaika na mauzo ya mshambuliaji huyo kwani mkataba wake na Yanga ulikuwa bado haujamalizika
Inaelezwa Makambo ameuzwa kwa dau linalokadiriwa kufikia Milioni 230 za Kitanzania




SIMBA YAIKUNG’UTA MTIBWA SUGAR BAO 3-0 UWANJA WA UHURU YATINGA KILELENI

Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba wameendelea kujiweka katika nafasi nzuri ya kutetea taji lao baada ya leo kuichapa Mtibwa Sugar mabao 3-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru

Simba iliingia kwenye mchezo huo ikiwa na shauku ya kuondoka na alama zote tatu baada ya kutopata ushindi katika michezo miwili iliyopita
Ilianza kuhesabu bao la kwanza kupitia kwa nahodha John Bocco kwenye dakika ya 32 akiunganisha krosi murua iliyochongwa na Meddie Kagere

Simba iliyotawala mchezo huo, ilikwenda mapumziko ikiwa inaongoza kwa bao 1-0

cut

Kasi waliyomaliza nayo kipindi cha kwanza, waliiendeleza kwenye kipindi cha pili na kufanikiwa kufunga mabao mengine mawili kupitia kwa Emmanuel Okwi(56′) na Clatous Chama (46′)
Mtibwa Sugar ilitumia zaidi mashambulizi ya kushitukiza na ilipoteza nafasi kadhaa kutokana na washambuliaji wake kutokuwa makini
Washambuliaji wa Simba wameendelea kuweka rekodi ya kuzifumania nyvu msimu huu, Simba ikifikisha mabao 72
Kagere, Bocco na Okwi wamefikisha mabao 50
Ushindi huo umeirejesha Simba kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 85
Simba sasa inahitaji alama nne tu kutoka mechi nne zilizobaki ili iweze kutetea ubingwa

Simba yaomba sapoti ya mashabiki mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar

Leo saa kumi jioni Simba itashuka uwanja wa Uhuru kuikabili Mtibwa Sugar katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara

Uongozi wa timu hiyo umewataka mashabiki wajitokeze kwa wingi kuwapa sapoti wachezaji katika mchezo huo ambao matokeo ya ushindi ni muhimu

Msemaji wa Simba Haji Manara amesema wachezaji wameahidi kupambana ili kupata matokeo lakini uwepo wa mashabiki wengi uwanjani itakuwa chachu ya wao kufanya juhudi zaidi

“Twendeni uwanjani kwa wingi kama ilivyo kawaida yetu. Tunahitaji alama nane tu tuweze kutwaa ubingwa, tujitokeze kwa wingi kwani kwa umoja wetu tutashinda”

Mchezo wa leo ni kwanza kwa Simba na Mtibwa Sugar kukutana msimu huu. Mchezo wa pili baina ya timu hizo utapigwa mkoani Morogoro, May 28