Mashabiki Mbeya kama kawaida uwanja wa Sokoine leo

Simba leo iko ugenini mkoani Mbeya ikiikabili Tanzania Prisons katika mchezo wa pili utakaopigwa uwanja wa Sokoine katika kipinci cha siku tatu

Lakini asikwambie mtu, mzuka wa mashabiki wa timu hiyo mkoani Mbeya, unawafanya mabingwa hao wa Tanzania Bara kutojihisi kabisa kama wako ugenini

Katika mchezo dhidi ya Mbeya City ambao Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-1, mashabiki wa ‘Mnyama’ walifunika dimba la Sokoine.

Leo tena wameahidi kuwa sambamba na timu yao kuhakikisha alama zote tatu zinakwenda Msimbazi

Mchezo unatarajiwa kuanza saa kumi kamili jioni na tayari mashabiki wameanza kujisogeza uwanja wa Sokoine

Simba yasaka alama nyingine tatu Mbeya

Baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mbeya City juzi, leo Simba inarejea tena uwanja wa Sokoine kuikabili Tanzania Prisons

Mchezo ambayo kama Simba itaibuka na ushindi, itasogea zaidi kileleni mwa msimamo wa kwani itabakisha alama mbili tu kuifikia Yanga

Meneja wa Simba Patrick Rweyemamu amesema wachezaji wa timu yake wako katika hali nzuri, wamejiandaa vyema kuweza kupata alama nyingine tatu leo

Tanzania Prisons ilitua mkoani Mbeya juzi ikitokea Dar es salaam ambako ilifungwa na Yanga mabao 2-1

Kocha Mkuu wa timu hiyo Adolph Richard amesema wanatarajia mchezo hautakuwa mwepesi lakini wamepania kupata matokeo ili kujiweka salama na hatari ya kuteremka daraja

Baada ya mchezo huo Simba itarejea jijini Dar es salaam ambako itakuwa na nafasi ya kutwaa ubingwa katika michezo sita itakayocheza uwanja wa Taifa/Uhuru

Esperance yatinga fainali ligi ya mabingwa, kucheza na Wydad Casablanca

Esperance imetinga fainali ligi ya mabingwa Barani Afrika baada ya kuiondosha TP Mazembe kwa ushindi wa bao 1-0

Esperance leo imeilazimisha TP Mazembe suluhu ya bila kufungana katika mchezo uliopigwa dimba la Mazembe, Lubumbashi huku ikitoka kushinda bao 1-0 kwenye mchezo wa kwanza

Mamelodi Sundowns pia imeshindwa kupindua matokeo ya 2-1 iliyofungwa na Wydad Casablanca kwenye mchezo wa kwanza baada ya kulazimishwa suluhu ya bila kufungana

Esperance imetinga fainali kwa msimu wa pili mfululizo sasa itachuana na Wydad Casablanca michezo miwili ya fainali itakayopigwa mwishoni mwa mwsi huu

Yanga yasogeza mbele Gala Dinner

Uongozi wa Yanga umeahirisha hafla ya chakula cha jioni (Gala Dinner) iliyokuwa limepangwa kufanyika Jumamosi ijayo, May 11 2019 ili kuwapa nafasi wadau wa klabu hiyo kushiriki katika mazishi ya Mwanachama wao marehemu Dk Reginald Mengi ambaye aliwahi kuifadhili Yanga miaka ya nyuma

Hafla hiyo sasa itafanyika May 18 Hoteli ya Serena jijini Dar es salaam

Mwili wa Dk Mengi unatarajiwa kuwasili Jumatatu ambapo utahifadhiwa kwenye nyumba yake ya milele Jumamosi ya May 11, Machame mkoani Kilimanjaro

Igangula ajitoa uchaguzi Yanga

Mgombea mwingine wa nafasi ya Mwenyekiti Baraka Igangula amejiondoa katika kinyan’ganyiro cha nafasi hiyo katika uchaguzi wa Yanga utakaofanyika kesho Jumapili

Inaelezwa Igangula ameamua kumuunga mkono Dk Mshindo Msolla ambaye sasa atachuana na Dk Jonas Tiboroha aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Yanga

Dk Msolla amepata uungwaji mkono mkubwa na anapewa nafasi kubwa ya kuibuka kidedea kwenye uchaguzi huo wa kesho

Yanga kupata viongozi wapya kesho

Wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi katika klabu ya Yanga leo wanahitimisha zoezi la kampeni kuelekea uchaguzi Mkuu wa klabu hiyo utakaofanyika kesho Jumapili ukumbi wa Bwalo la Polisi, Osterbay jijini Dar es salaam

Wagombea walianza kunadi sera zao kwa Wanachama Jumanne iliyopita

Nafasi ya Mwenyekiti wa Yanga inawaniwa na wagombea watatu Barak Igangula, Dk Jonas Tiboroha na Dk Mshindo Msolla wakati nafasi ya Makamu Mwenyekiti inawaniwa na wagombea wanne ambao ni Fredrick Mwakalebela, Janeth Mbene, Titus Osoro na Yono Kevela

Aidha wagombea 21 wanawania nafasi nane za wajumbe wa Kamati ya Utendaji

Wanachama wa Yanga wametakiwa kutofanya makosa kwenye uchaguzi wa kesho kwa kuwachagua viongozi ambao wataweza kuipeleka Yanga mbele

Suala la Mabadiliko limekuwa kilio cha Wanayanga. Wagombea wote wameahidi kufanya mabadiliko, ni jukumu la Wanachama kujiridhisha na uwezo wao na ahadi walizotoa katika kutatua changamoto zinazoikabili Yanga

Wanachama wameaswa kutochagua viongozi kwa mazoea badala yake wachague viongozi ambao wana upeo mkubwa

Ni vyema kiongozi atakayechaguliwa awe na uwezo wa kutengeneza mikakati ya kuipeleka Yanga kule ambako kila mdau anahitaji kuona klabu ikielekea

Huu sio wakati wa kujaribu viongozi, Wanachama wawaweke madarakani ‘watu wa kazi’

Wanachama wasichague viongozi kwa papara, mihemko na makundi, kila mmoja afanye uamuzi kwa maslahi ya klabu kwa kuchagua viongozi wenye tija

Yanga ikipata viongozi wazuri, utakuwa mwanzo wa kutengeneza Yanga imara ambayo itagombewa na wawekezaji na kuifanya timu hiyo kongwe zaidi Tanzania kuondokana na dimbwi la ‘umasikini’