
Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amethibitisha kuwa Nyoni hatakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kitakachoshuka dimbani kuikabili Alliance Fc
Nyoni anaungana na beki Paschal Wawa ambaye hakusafiri jijini Mwanza kutokana na majeruhi yanayomkabili

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amethibitisha kuwa Nyoni hatakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kitakachoshuka dimbani kuikabili Alliance Fc
Nyoni anaungana na beki Paschal Wawa ambaye hakusafiri jijini Mwanza kutokana na majeruhi yanayomkabili

Mchezo huo utapigwa kesho Jumanne, April 23 katika uwanja huo
Simba ilitua Mwanza mapema jana ikitokea Kagera ambako ilipoteza mchezo dhidi ya Kagera Sugar kwa kuchapwa mabao 2-1
Katika mazoezi hayo yaliyosimamiwa na kocha Patrick Aussems, Simba iliwaruhusu kukaa jukwaani mashabiki waliofika kuwashuhudia mabingwa hao watetezi
Kuelekea mchezo huo, Aussems amesema wanatarajia kupata upinzani mkali kutoka kwa Alliance Fc kutokana na ubora wa kikosi cha timu hiyo
Hata hivyo amesema Simba inahitaji kushinda mchezo huo hasa baada ya kupoteza mchezo uliopita
“Tunajua haitakuwa mechi rahisi sababu Alliance ni timu nzuri lakini sisi tumepoteza mchezo Bukoba na kesho tunataka alama tatu,” amesema Aussems
“Tunajua kwanini tulipoteza na tumejiandaa kwa hilo na ninaamini kesho tutakuwa vizuri.”

Magoli ya Simba Queens yalipachikwa na Opah Clement aliyefunga mabao mawili, Mwanahamisi Omary, Joele Bukulu na Amina Ramadhani na goli pekee la Yanga Princess likifungwa na Fausta Thomas
Huu ni ushindi wa pili kwa Simba Queens dhidi ya watani zao, wakipata ushindi wa mabao 7-0 katika mchezo wa duru ya kwanza wa ligi hiyo ya Wanawake

Simba imedhamiria kuanza mapema maboresho ya kikosi chake ambapo imebainika mikataba ya nyota zaidi ya 10 inamalizika mwishoni mwa msimu
Baadhi ya wachezaji ambao mikataba yao inaelekea ukiongoni ni pamoja na John Bocco, Emmanuel Okwi, Haruna Niyonzima, Erasto Nyoni, Aishi Manula, Shomari Kapombe, Paschal Wawa, Paul Bukaba, James Kotei, Asante Kwasi na Nicolas Gyan
Imeelezwa hatma ya wachezaji hao inasubiri mapendekezo ya Aussems ambaye ndiye aliyeachiwa jukumu zima la usajili huku uongozi wa Simba ukibaki katika utekelezaji
Hata hivyo idadi kubwa ya wachezaji hao wataendelea kubaki Msimbazi kutokana na mchango mkubwa waliotoa msimu huu
Afisa Mtendaji Mkuu wa Simba Crescentius Magori amesema hawatarajii kukivuruga kikosi chao ambacho kimefanya vizuri msimu huu lakini watasikiliza kile kitakachopendekezwa na Aussems kwa ajili ya maboresho
“Masuala yote ya usajili Simba mwenye kauli ya mwisho ni kocha. Tunafahamu baadhi ya nyota wetu mikataba yao inamalizika, hata hivyo mpaka sasa hakuna mchezaji ambaye kocha amesema tumuache, hivyo tutawapa mikataba mipya,” amesema Magori
Baada ya Simba kuondoshwa hatua ya robo fainali michuano ya Ligi ya Mabingwa, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Simba, Mohammed Dewji ‘MO’ alisema msimu ujao wanataka kuwa na kikosi imara zaidi na hawatasita kuachana na wachezaji ambao mchango wao ni mdogo au watovu wa nidhamu

Simba Queens inayoshika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi hiyo, imepania kuendeleza umwamba dhidi ya wapinzani wao hao ambao wanashika nafasi ya saba
Katika mchezo wa raundi ya kwanza Simba Queens iliibamiza Yanga Princess mabao 7-0
JKT Queens inaongoza ligi ikiwa imejikusanyia alama 45 ikiwa imeshinda michezo yake yote.
Mlandizi Queens inashika nafasi ya pili ikiwa imejikusanyia alama 32 sawa na Alliance Girls timu hizo zikitofautiana mabao ya kufunga na kufungwa
Simba Queens iko nafasi ya nne ikiwa na alama 31 wakati Yanga Princess inashika nafasi ya saba ikiwa na alama 19
Aussems amekamilisha sharti la kwanza na kuvuka malengo baada ya kufanikiwa kuivusha Simba hadi robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa
Sharti lililobaki ni la kutetea ubingwa wa ligi kuu, sharti ambalo nalo anaelekea kulikamilisha
Mbelgiji huyo aliyechukua nafasi ya Pierre Lechantre, hakuna shaka atapewa mkataba mpya kuendelea kuinoa Simba kutokana na mafanikio aliyoipatia timu hiyo msimu huu
Mkataba wake na Simba aliosaini msimu uliopatita utamalizika mwishoni mwa msimu

Kocha Mkuu wa vinara hao wa ligi Mwinyi Zahera aliwapa wachezaji siku tatu za mapumziko ili washeherekee sikukuu ya Pasaka wakiwa na familia zao
Mratibu wa Yanga Hafidh Saleh amesema baada ya mapumziko hayo, kesho wataanza kujifua uwanja wa Chuo cha Polisi, Kurasini kujiandaa na mchezo huo
Yanga bado haijakata tamaa katika mbio za kuwania ubingwa licha ya watani zao Simba kuwa na idadi kubwa ya michezo ya viporo ambayo kama watashinda yote, watatetea ubingwa waliotwaa msimu uliopita
Juzi Zahera alisema hesabu zao ni kushinda michezo yote sita iliyobaki huku akiamini wapinzani wao Simba wataendelea kudondosha pointi hivyo kuwapa mwanya wa kutwaa ubingwa
Yanga iko kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa imejukusanyia alama 74 baada ya kushuka dimbani mara 32.
Inafuatiwa na Azam Fc yenye alama 66 ikiwa imeshuka dimbani mara 32 pia. Simba inashika nafasi ya tatu ikiwa na alama 60 ilizovuna katika michezo 24


















Mchezo huo utapigwa keshokutwa, April 23 2019 katika uwanja wa CCM Kirumba



