RATIBA: Mechi za Leo Tpl

Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo inaingia mzunguuko wa 31 kwa michezo mitatu kupigwa

Vinara wa ligi hiyo Yanga wao watashuka dimbani mkoani Iringa kesho Jumamosi kuikabili Lipuli Fc katika mchezo ambao matokeo ya ushindi yatazidi kuin’garisha timu hiyo kileleni

Aussems afunguka utayari wa kikosi cha Simba kuelekea mchezo wa kesho

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema vijana wake wako tayari kuwakabili AS Vita Club na hawana wasiwasi wowote kuelekea mchezo huo

Jana jioni Simba ilijifua katika uwanja wa Taifa yakiwa ni maandalizi yake ya mwisho katika uwanja huo kabla ya mchezo hapo kesho

Aussems amesema licha ya kuwa tayari wamefikia malengo ya msimu huu ya kutinga hatua ya makundi, lakini wana nafasi adimu ya kutinga robo fainali kama watashinda mchezo huo utakaopigwa mbele ya mashabiki wake takribani elfu 60

“Mimi nipo sawa na hata wachezaji wangu wapo vizuri, ni mechi yenye msisimko sana tunajua tukishinda tutaingia robo fainali na tumesubiri jambo hili kwa miezi 7 sasa,” amesema

“Hata kama matarajio hayakuwa makubwa sisi kufika mbali kwenye ligi ya mabingwa Afrika, lakini bado tuna nafasi kwa hiyo hatuna presha, zaidi presha ipo kwao (AS Vita) kwa sababu ni wanafainali wa kombe la shirikisho mwaka jana na kama hawatafuzu itakuwa jambo baya sana kwao.”

“Hatupo katika hali inayofanana, chochote kitakachotokea ni ziafa kwetu, tuna nafasi adimu ya kucheza mchezo huu muhimu mbele ya mashabiki 60,000 kwa hiyo itakuwa mechi nzuri na wachezaji wapo tayari.”

Mchezo huo utapigwa saa moja usiku sambamba na mchezo kati Al Ahly dhidi ya JS Saoura

Mzee Akilimali augua Bagamoyo

Hali ya Mwanachama maarufu wa klabu ya Yanga Mzee Ibrahim Akilimali inaelezwa sio nzuri ambapo amelazwa Hospitali ya Baobab akiendelea na matibabu ya ugonjwa kisukari

Mzee Akilimali amewaomba wadau wa Yanga na Watanzania wote kwa ujumla wamuombee ili aweze kupona maradhi yanayomsumbua

“Hali yangu sio nzuri. Niko huku Bagamoyo najiuguza maradhi ya kisukari. Mniombee kwani kisukari kinanitesa sana,” Mzee Akilimali amenukuliwa na Spoti Xtra

Mzee Akilimali ni miongoni mwa wanachama wa Yanga vinara wa kutoa maoni juu ya masuala mbalimbali ya klabu hiyo

Wakati mwingine hujikuta akiingia katika mgogoro na wanachama wenzake, wakimtuhumu kuwa ni mpinga maendeleo.

Djuma aitakia kheri Simba

Kocha Mkuu wa AS Kigali inayoshiriki ligi kuu ya Rwanda, Masudi Djuma ameitakia kheri Simba ili iweze kushinda mchezo dhidi ya AS Vita Club na kuweza kutinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Djuma aliyewahi kuhudumu Simba akiwa kocha msaidizi kwa misimu miwili, amesema Simba itakayokuwa nyumbani ina kila sababu ya kushinda mchezo huo Jumamosi

“Timu zinazoshiriki michuano ya ligi ya mabingwa msimu huu zimetumia vyema viwanja vyao vya nyumbani. Naamini Simba itatumia uwanja wake vizuri pia,” Djuma aliiambia Radio eFM

Djuma aliondolewa Simba mwezi Oktoba mwaka jana baada ya kutofautiana na kocha Mkuu Patrick Aussems.

Nafasi yake tayari imechukuliwa na kocha Denis Kitambi

Djuma anabaki kuwa miongoni mwa makocha waliopita Simba na kukubalika sana na mashabiki wa timu hiyo

Okwi, Nyoni wanogesha mazoezi Simba

Kiraka Erasto Nyoni na mshambuliaji Emmanuel Okwi leo walikuwepo uwanjani wakijifua na kikosi cha Simba kinachojiandaa na mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya AS Vita takaopigwa Jumamosi, March 16 katika uwanja wa Taifa

Simba iliyorejea jana kutoka Algeria inajifua kwenye uwanja wa Boko Veterans

Nyoni na Okwi hawakusafiri na Simba ilipokwenda nchini Algeria kumenyana na JS Saoura kutokana na kuwa majeruhi

Wachezaji hao leo wamejumuika na wachezaji wengine wakihusika katika program zote za mazoezi hivyo kuongeza matumaini kuwa wako tayari kwa ajili ya mchezo wa Jumamosi