
Washambuliaji hao hatari wa Simba wamefunga mabao matatu kila mmoja katika mchezo dhidi ya Coastal Union uliomalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa mabao 8-1
Mwamuzi wa mchezo huo Jonesia Rikiyaa aliwakabidhi mpira kila mmoja baada ya mchezo kumalizika
Hizo zilikuwa hat-trik za sita kufungwa kwenye ligi msimu huu
Kagere amefikisha mabao 20 na kujiimarisha kileleni katika mbio za kuwania kiatu cha dhahabu akiwaacha Heritier Makambo na Salim Aiyee wakibaki na mabao 16
Okwi mfungaji bora wa ligi msimu uliopita, amerejea katika mbio za kuwania kiatu hicho baada ya leo kufikisha mabao 14 akimfikisha mshambuliaji mwingine wa Simba John Bocco
Kagere, Okwi na Bocco wameifungia Simba mabao 48 kwa pamoja
































