
Bocco aliyetua Simba akitokea klabu ya Azam Fc ambayo aliitumikia kwa takribani miaka 10, nidye kinara wa muda wote wa upachikaji mabao katika ligi ya Tanzania akiwa amefunga mabao zaidi ya 100
Licha ya umri kusonga, Bocco ‘hachuji’, ameendelea kuwa katika ubora uleule wa kupachika mabao
Msimu huu ameifungia Simba mabao 14 kwenye ligi akishika nafasi ya nne katika orodha ya vinara wa upachikaji mabao nyuma ya Meddie Kagere (16), Salim Aiyee (16) na Heritier Makambo (15)
Msimu uliopita Bocco aliifungia Simba mabao 14 na kushika nafasi ya pili nyuma ya Emmanuel Okwi ambaye msimu huu kasi yake ya kuzifumania nyavu imepungua akiwa amefunga mabao 10
Bocco kwa kushirikiana na Kagere na Okwi, wamefungia Simba jumla ya mabao 40 kwenye ligi msimu huu na kuifanya Simba kuwa moto wa kuotea mbali katika kuzifumania nyavu ikiwa imefunga jumla ya mabao 57















