Misimu miwili, mabao 35 huyu ndio John Bocco

Nahodha wa Simba John Bocco amefikisha mabao 35 katika misimu miwili aliyoitumikia Simba kwenye mashindano yote

Bocco aliyetua Simba akitokea klabu ya Azam Fc ambayo aliitumikia kwa takribani miaka 10, nidye kinara wa muda wote wa upachikaji mabao katika ligi ya Tanzania akiwa amefunga mabao zaidi ya 100

Licha ya umri kusonga, Bocco ‘hachuji’, ameendelea kuwa katika ubora uleule wa kupachika mabao

Msimu huu ameifungia Simba mabao 14 kwenye ligi akishika nafasi ya nne katika orodha ya vinara wa upachikaji mabao nyuma ya Meddie Kagere (16), Salim Aiyee (16) na Heritier Makambo (15)

Msimu uliopita Bocco aliifungia Simba mabao 14 na kushika nafasi ya pili nyuma ya Emmanuel Okwi ambaye msimu huu kasi yake ya kuzifumania nyavu imepungua akiwa amefunga mabao 10

Bocco kwa kushirikiana na Kagere na Okwi, wamefungia Simba jumla ya mabao 40 kwenye ligi msimu huu na kuifanya Simba kuwa moto wa kuotea mbali katika kuzifumania nyavu ikiwa imefunga jumla ya mabao 57

Aussems anataka ushindi mechi zote zilizobaki

Kikosi cha Simba tayari kimerejea jijini Dar es salaam baada ya kumaliza ratiba ya michezo ya kanda ya ziwa

Simba kesho Jumanne itashuka uwanja wa Uhuru kuikabili JKT Tanzania katika mchezo mwingine wa ligi kuu ya Tanzania Bara

Kocha Mkuu wa mabingwa hao watetezi Patrick Aussems amesema licha ya timu yake kukusanya alama tisa kutoka kanda ya ziwa, bado kazi haijamalizika na wanahitaji kushinda michezo yote iliyobaki waweze kutetea ubingwa wao

Aidha Aussem amesema ushindani kwenye ligi umeongezeka katika kipindi hiki cha lala salama hivyo wanahitaji kupambana kila mara wanaposhuka dimbani

“Bado tuna kazi ya kufanya, mechi zote ni ngumu, ligi bado ina ushindani, hakuna mechi rahisi, kila timu inahitaji ushindi ndio maana hakuna anayekata tamaa mpaka filimbi ya mwisho inapopigwa, tunataka kushinda kila mechi iliyopo mbele, ” amesema

Baada ya mchezo dhidi ya JKT Tanzania kesho, kikosi cha Simba kitaelekea mkoani Mbeya ambako kitacheza michezo miwili dhidi ya Mbeya City na Tanzania Prisons

Kimahesabu, Simba inahitaji kushinda michezo nane kati ya 11 iliyobaki ili kujihakikishia ubingwa bila ya kujali matokeo ya mpinzani wake Yanga ambaye leo huenda akadondosha pointi zaidi dhidi ya Azam Fc

Kapombe anakaribia kurejea kisosini Simba

Uongozi wa Simba umethibitisha kuwa beki wake kiraka Shomari Kapombe anakaribia kurejea kikosini baada ya kuanza mazoezi mepesi

Msemaji wa Simba Haji Manara amesema Kapombe amepona majeraha ya goti na tayari ameanza mazoezi ya gym ikiwa ni hatua ya mwanzo kabla ya kurejea dimbani

“Tunashukuru beki wetu Shomari Kapombe amepona majeraha ya goti yaliyomuweka nje kwa muda mrefu. Hivi sasa anafanya mazoezi ya Gym ili kuurejesha mwili katika hali yake kabla ya kuanza mazoezi ya mpira,” amesema

Kapombe amekuwa nje kwa zaidi ya miezi mitano akiuguza majeraha ya goti aliyopata nchini Afrika Kusini wakati akiitumikia timu ya Taifa

Licha ya beki huyo kuanza kujifua, kuna uwezekano mdogo kwake kucheza mechi zilizobaki

Simba yaondoka Mwanza kurejea Dar

Kikosi cha Simba kimeondoka leo jijini Mwanza kurejea jijini Dar es salaam kuendelea na ratiba ya michezo ya ligi kuu ambapo keshokutwa Jumanne itachuana na JKT Tanzania katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Uhuru

Simba imemaliza salama ratiba ya michezo ya kanda ya ziwa ikifanikiwa kushinda michezo mitatu na kufungwa mchezo mmoja

Baada ya mchezo dhidi ya JKT Tanzania, kikosi cha Simba kitaelekea mkoani Mbeya kuzifuata Mbeya City na Tanzania Prisons

Simba yaondoka Mwanza kurejea Dar

Kikosi cha Simba kimeondoka leo jijini Mwanza kurejea jijini Dar es salaam kuendelea na ratiba ya michezo ya ligi kuu ambapo keshokutwa Jumanne itachuana na JKT Tanzania katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Uhuru

Simba imemaliza salama ratiba ya michezo ya kanda ya ziwa ikifanikiwa kushinda michezo mitatu na kufungwa mchezo mmoja

Baada ya mchezo dhidi ya JKT Tanzania, kikosi cha Simba kitaelekea mkoani Mbeya kuzifuata Mbeya City na Tanzania Prisons

Wanaosema Simba ‘inabebwa’ wajitafakari

Afisa Habari wa Simba Haji Manara amewashangaa mashabiki wanaosema klabu hiyo inabebwa na waamuzi wakati timu hiyo imepata mafanikio nje na ndani ya Tanzania kutokana na ubora wa kikosi chake

Manara amesema Simba imekuwa ikicheza kila baada ya siku mbili na inapata matokeo kutokana na ubora wake na si vinginevyo

“Tumefika robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa tulibebwa na nani?” alihoji Manara

“Hata hao Yanga ambao mashabiki wao wanalalamika kuwa tunabebwa nao tuliwafunga, je tulibebwa?”

“Kwa sasa Simba ndio timu yenye kikosi bora Tanzania, ndio mabingwa watetezi na baada ya wiki moja tutakuwa kileleni mwa msimamo wa ligi tayari kurejesha ubingwa Msimbazi”

Simba imebakisha michezo 11, lakini inahitaji kushinda michezo nane tu ili iweze kutwaa ubingwa

Aidha kama Yanga itashindwa kuifunga Azam Fc kesho, Simba itahitaji kushinda michezo miwili tu ili kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi

Aussems ashangazwa na mzuka wa mashabiki Musoma

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amewashukuru mashabiki wa timu hiyo mkoani Mara kwa sapoti waliyotoa kwa mabingwa hao watarajiwa wa ligi kuu kwa msimu wa pili mfululizo

Aussems amesema amefarijika kuona mashabiki wakijitokeza kwa wingi uwanjani jana lakini zaidi juzi Simba ilipotua mkoani Mara

“Tumefarijika na mapokezi waliyotupa mashabiki wa hapa ikiwa ni muda mrefu umepita tangu Simba ije kucheza hapa,” amesema

“Tumewaachia zawadi ya ushindi, sisi tunaelekea Dar ambako tutacheza mchezo mmoja Jumanne (na JKT Tanzania) kisha tutaelekea mkoani Mbeya kuzikabili Mbeya City na Tanzania Prisons”

Msafara wa Simba ulilala jijini Mwanza ambapo leo wanarejea jijini Dar es salaam kwa usafiri wa ndege

Niyonzima aomba radhi

Kiungo fundi Haruna Niyonzima amewaomba radhi kwa uongozi wa klabu ya Simba pamoja na mashabiki wa timu hiyo kufuatia kadi nyekundu aliyopewa kwenye mchezo wa jana dhidi ya Biashara United, mchezo ambao Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-0

Niyonzima amesema anajutia tukio alilofanya ambalo lilisababisha apewe kadi nyekundu

“Ulikua mchezo wenye presha kubwa sana ukizingatia tulihitaji sana matokeo kuliko chochote,” amesema

“Iliniumiza sana kutoka uwanjani nikiacha timu yangu pungufu. Niombe radhi kwa klabu yangu mashabiki zetu waliosafiri mpaka Mara na pia wale wote mliokua majumbani mkitizama kupitia televisheni”

“Nilichofanya hakikuwa bora kwa ustawi wa mpira wetu samahani wote mliokwazika, tutapambana mpaka tone la mwisho kwajili ya ubingwa”

Mashabiki wa Simba Mara ‘mmetisha’

Mapokezi na sapoti iliyopata Simba mkoani Mara ni ya kipekee na hakika watu wa Musoma wanastahili pongezi kwa ‘vibe’ la maana waliloonyesha leo

Simba haikuwa imefika Mara katika kipindi cha miaka 15 kutokana na mkoa huo kukosa timu ya ligi kuu, makaribisho iliyopata yanadhihirisha ukubwa wa Simba nchini Tanzania kwa sasa

Baada ya mchezo wa leo kikosi cha Simba kinatarajiwa kuondoka kesho kurejea jijini Dar es salaam kujiandaa na mchezo unaofuata dhidi ya JKT Tanzania

FT : Biashara United 0-2 Simba

Simba imeendeleza umwamba wake kwenye ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya leo kuifumua Biashara United mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Karume, Mara

Simba imefikisha alama 69 sasa ikitofautiana na Yanga kwa tofauti ya alama tano tu huku kibindoni ikiwa na michezo mitano ya viporo

Shukrani za kipekee zimwendee nahodha John Bocco aliyefunga mabao yote mawili kwenye kipindi cha kwanza na kuihakikishia Simba alama tatu muhimu

Bocco amefikisha mabao 14 akichupa mpaka nafasi ya tatu kwenye orodha ya vinara wa mabao nyuma ya Makambo mwenye mabao 15

Aidha Bocco amefikisha idadi ya mabao aliyofunga msimu uiliopita

Katika mchezo huo Simba ilipata pigo baada ya kiungo wake Haruna Niyonzima kutolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumtolea maneno machafu mwamuzi

Simba imemaliza michezo ya kanda ya ziwa na sasa inarejea jijini Dar es salaam ambapo Jumanne itachuana na JKT Tanzania, mchezo utakaopigwa uwanja wa Uhuru