Kumbuka kubonyeza X au kitufe cha kurudi nyuma endapo utaona matangazo.
ITAZAME MECHI YA REAL MADRID VS ATHLETIC BILBAO LIVE HAPA
Kumbuka kubonyeza X au kitufe cha kurudi nyuma endapo utaona matangazo.
Kauli ya Zahera imekuja kufuatia Manara kumsema kocha huyo kuwa amekuwa akiishutumu bodi ya ligi na TFF kuwa inafanya mpango wa kuiwezesha Simba kuchukua ubingwa wa ligi.
Ameeleza kwa kumtaka Manara ni vema akafuatilia mambo yanayomhusu na kuachana na kumzunguzia yeye kwani anaona anachokifanya ni sahihi.
Zahera amesema kamwe hatoweza kukaa kimya kwani kila anachokisema ni sahihi kwake na hataweza kufumbia macho madudu ya TFF.
Amefunguka kwa kusema kama TFF wanaona anakiuka taratibu wamfungie lakini hatoacha kuzungumza mpaka pale uongozi wa Shirikisho hilo utakapobadilika.

Aidha matokeo hayo yametoa taswira kuwa haitakuwa kazi rahisi kwa Simba kushinda michezo yote iliyobaki
Kama Yanga itashinda michezo yote sita iliyobaki itafikisha alama 92 huku wapinzani wao wakiwa na mzigo wa kupata matokeo kwenye michezo 14 ndani ya mwezi mmoja
Yanga imeendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa imejikusanyia alama 74 ikifuatiwa na Azam Fc yenye alama 66
Simba ni ya tatu ikiwa na alama 60
Azam na Yanga zimeshuka dimbani mara 32 wakati Simba imeshuka dimbani mara 24
Simba inakabiliwa na ratiba ngumu ya michezo ya viporo ambapo katika kipindi cha siku 15 itashuka dimbani mara sita

Keshokutwa April 23 Simba itashuka uwanja wa CCM Kirumba kuchuana na Alliance Fc na siku mbili baadae, April 25 Simba itarejea kwenye uwanja huo kuchuana na KMC kisha kikosi cha mabingwa hao watetezi kitaelekea mkoani Mara kuikabili Biashara United April 28


Kagera Sugar ilikuwa bora zaidi kwenye kipindi cha kwanza ambapo ilipachika mabao yake mawili yaliyofungwa na Kassim Khamis na Ramadhani Kapera
Simba ilikuja juu kwenye kipindi cha pili na kufanikiwa kufunga bao lake kupitia kwa Emmanuel Okwi kwenye dakika ya 64
Wekundu wa Msimbazi walikosa nafasi kadhaa ambazo zingewawezesha kuondoka na angalau alama moja dhidi ya Kagera Sugar ambayo kwa mara nyingine imedhihirisha umwamba wake dhidi ya Simba
Simba haikuwa katika kiwango bora leo, pengine uchovu uliosababishwa na timu kucheza mfululizo umechangia kukosa matokeo muhimu
Baada ya mchezo huo Simba inaelekea mkoani Mwanza ambapo Jumanne, April 23 itacheza na Alliance Fc

Maadhimisho hayo yatakwenda sambamba na ibada kwenye makanisa mbalimbali nchini pamoja na burudani zitakazofanyika kumbi tofauti za starehe, fukwe za bahari na sehemu nyingine.
Sherehe hii ambayo kwa Wakristo huwakumbusha upendo, inatakiwa kusherehekewa katika hali ya amani na utulivu.
Tunawatakia Wanamsimbazi na Watanzania wote Pasaka Njema.

“Nawapongeza Kagera Sugar kwa sababu walikuwa na mchezo mzuri katika kipindi cha kwanza, sisi hatukuwa bora,” alizungumza Aussems baada ya mchezo jana
“Walitumia udhaifu wetu kuweza kufunga mabao mawili ambayo kwetu haikuwa rahisi kuyarejesha yote kwenye kipindi cha pili licha ya kurekebisha makosa tuliyofanya kwenye kipindi cha kwanza”
“Wachezaji wangu walicheza dakika 45 za kipindi cha pili na kufanikiwa kufunga bao moja na kutengeneza nafasi nyingine ambao tulishindwa kuzitumia. Hata hivyo mchezo ni dakika 90”
Baada ya mapumziko ya Pasaka, Simba itaelekea mkoani Mwanza kuikabili Alliance Fc kwenye mchezo mwingine wa ligi utakaopigwa keshokutwa April 23 katika dimba la CCM Kirumba