TETESI Za Usajili Ulaya

TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO IJUMAA NOV 23, 2018.

1.ARSENAL inamnyatia nyota kinda wa As Roma Mturuki, Cengiz Under ambaye pia anatakiwa na Manchester City. (#Calciomercato).

2.ARSENAL pia inamtaka Kiungo wa Borussia Dortmund, Julian Weigl. (#SportsBild).

3.SEVILLA itamnunua jumla Mshambuliaji wa Ureno, Andre Silva kwa pauni €35m ambaye anaichezea kwa mkopo klabu hiyo kutoka Ac Milan.(#Goal).

4.JUVENTUS inataka huduma ya Kiungo Mshambuliaji wa Wolves, Ruben Neves. (#Tuttosport).

5.CHELSEA imeungana na Manchester United kuisaka saini ya Beki wa kati wa Inter Milan, Milan Skriniar mwenye thamani ya pauni £70m. (#TheSun).

6.MSHAMBULIAJI wa Manchester United, Marcus Rashford ameripotiwa ataanza mazungumzo na Real Madrid ya kuhamia Santiago Bernabeu. #TheSun imeripoti.

7.HOFFENHEIM inamtaka Mshambuliaji wa Brighton, Aaron Connolly. (#SkySportNews).

8.PSG imeungana na Man City pamoja na Barcelona kuiwania saini ya Kiungo wa Ajax, Frenkie De Jong. (#Sport).

9.WEST HAM inataka kumsajili Mshambuliaji wa Bayern Munich, Sandro Wagner. (#TheSun).

10.KOCHA wa Man United, Jose Mourinho anawasaka Beki wa Atletico Madrid, Diego Godin, Gary Cahill na Kiungo wa As Roma, Lorenzo Pellegrin. Mreno huyo inadaiwa amepewa pauni£300m za usajili katika dirisha la January. (#DailyStar).

10.REAL MADRID itajaribu kuisaka saini ya Mshambuliaji wa Inter Milan, Mauro Icardi katika dirisha la January. (#OKdiario).

11.REAL MADRID imerudi tena ufaransa ikimtaka Fowadi wa PSG, Neymar huku Mbrazil huyo akifungua milango ya kurudi Barcelona. (#COPE).

12. REAL MADRID itamtoa Winga wake, Gareth Bale pamoja na pauni €100m kwa Chelsea kama chambo ya kumnasa Eden Hazard. (#OKDiario).

13.ARSENAL itamtumia Fowadi wake, Pierre Aubameyang ili amshawishi Winga wa Barcelona, Ousmane Dembele ajiunge Emirates. (#Sport).

Man U: kumuongeza mkataba beki Huyu

Klabu ya Manchester United inatarajia kuanza mazungumzo na beki wake Chris Smalling ili kumuongezea mkataba mpya wa muda mrefu. .
.
Kwa mujibu wa taarifa zilizoripotiwa na mtandao wa Daily Mail zinasema mkataba huo utamfanya Smalling alipwe kiasi cha £120K kwa wiki. .
#sokaoUpdates

USAJILI: Tanzania Prisons Yapanga Kuimarisha..

Tanzania Prisons ipo kwenye mikakati ya kuimarisha safu yake ya ushambuliaji katika kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili.
:
Katibu wa timu hiyo Havinitishi Abdallah amesema miongoni mwa wachezaji wanaowataka ni pamoja na mshambuliaji wao wa zamani Mohamed Rashid ambaye kwa sasa yupo Simba.
:
“Tunajipanga kwenye dirisha dogo ili kufanya vizuri kwa sababu ukiangalia tatizo lipo kwenye ushbuliaji ndio tunataka kuongezea kwenye maeneo hayo kwa hiyo baada ya siku mbili tatu tutasema kitu kwa sababu tayari tumeanza mazungumzo na vilabu kutupa wachezaji kwa mkopo.
:
“Kuna wachezaji wapo Azam mwingine ni Mohamed Rashid yupo Simba, hivyo tunasubiri ndugu zetu watujibu na taarifa tumeshapeleka kuwaomba kwa mkopo.”
:
“Timu yetu siyo mbaya, inacheza vizuri na kutengeneza sana nafasi tatizo lipo kwenye kufunga na ndio tunalifanyia kazi. Sehemu nyingine zipo sawa.”

MOURINHO: Kuwapiga Bei Mabeki Hawa

#TetesiZaUsajili Baada ya taarifa za awali kudai kuwa kocha wa Manchester United Jose Mourinho yupo tayari kuwapiga bei beki wake Marcos Rojo pamoja na Eric Baily ili kusajili beki mwingine, klabu ya PSG inataka kutumia nafasi hiyo ili kumnasa Eric Baily kipindi cha usajili wa dirisha dogo mwezi January (The Mail)

C&p #sokaonlineUpdates

USAJILI: Yanga kushusha Kifaa Hiki Kutoka UGANDA

Taarifa za uhakika ni kwamba Yanga imekamilisha mazungumzo na mshambuliaji wa Kimataifa wa Uganda Nelson Senkatuka anayechezea Bright Stars inayoshiriki ligi kuu nchini humo.

Senkatuka anatarajiwa kutua nchini wiki ijayo ili kukamilisha taratibu za usajili tayari kuanza kuwatumikia mabingwa hao wa kihistoria wa Tanzania.

Msimu uliopita Senkatuka aliifungia Brights Stars mabao 18 kwenye ligi kuu ya Uganda.

Mabosi wa Kamati ya usajili ya Yanga wako ‘busy’ kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili kuhakikisha wanaongeza nguvu kwenye kikosi cha timu hiyo ambacho kinashika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi