KAIZER CHIEF YAMNYEMELEA OKWII

Wachezaji waandamizi wa kikosi cha Simba wameanza kunyemelewa kwa kasi na timu vigogo barani Afrika kutokana na kiwango kikubwa wanachoonyesha sasa.

Baada ya klabu za AS Vital na Zamalek kujitosa kumuwania Meddie Kagere, Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini nayo imejitosa kumuwania Emmanuel Okwi kulingana na Mwanaspoti

Chiefs ambayo iko visiwani Zanzibar kurudiana na Zimamoto kwenye mchezo wa kombe la Shirikisho, inadaiwa kutuma ofa ikitaka kumsajili kinara huyo wa mabao wa kikosi cha Simba

Okwi alirejea Simba msimu uliopita na katika msimu wake wa kwanza alifanikiwa kuwa mfungaji bora baada ya kufunga mabao 20.

Msimu huu tayari ameifungia Simba mabao saba akiwa nyuma ya Eliudi Ambokile wa Mbeya City anayeongoza na mabao tisa.

Uongozi wa Simba utakazimikia kufanya kazi ya ziada kuhakikisha washambuliaji wake hawachukuliwi na timu nyingine

Kwani ili kuweza kufikia malengo ya kuifanya Simba kuwa bingwa wa Afrika inahitaji kuwa na wachezaji hawa ambao tayari wameonyesha uwezo usio na shaka

Coulibaly Amwaga Wino MSIMBAZI

Klabu ya Simba imekamilisha usajili wa beki wa kulia Zana Coulibaly kutoka klabu ya Asec Mimosas ya ivory Coast.

Coulibaly aliyefuzu vipimo vya afya jana amesaini mkataba wa miaka miwili kuwatumikia mabingwa hao wa Tanzania Bara.

Coulibaly raia wa Burkina Faso amesajiliwa rasmi leo Ijumaa mchana na alikabidhiwa uzi wa Simba na kocha Mkuu Patrick Aussems mbele ya Mkurugenzi Mtendaji wa Simba Cresentius Magori

USAJILI: Simba yamsajili beki huyu

Simba imemnasa beki wa kulia wa klabu ya Asec Mimosas Zana Coulibaly.

Mchezaji huyo atawasili nchini leo kwa ajili ya kukamilisha taratibu za usajili.

Beki huyo anatarajiwa kuziba pengo la Shomari Kapombe ambaye atakuwa nje kwa muda mrefu baada ya kupata majeraha wakati akiitumikia timu ya Taifa

“Tunapenda kuwatangazia kwamba beki Zana Coulibaly kutoka ASEC Mimosas ya Ivory Coast leo atawasili nchini kwa ajili kukamilisha taratibu za mwisho kujiunga na timu yetu ili kuziba pengo la beki Shomari Kapombe ambaye siku za karibuni alipata majeraha,” imesema taarifa ya Simba

USAJILI: Simba kumsajili mchezaji huyu?

Mapema leo katika ukurasa rasmi wa klabu ya Simba mtandao wa Instagram iliwekwa picha ya beki kutoka klabu ya Asec Mimosas, Zana Oumar Coulibaly

Coulibaly ni mlinzi wa kulia anayetarajiwa kusajili na Simba kuziba pengo la Shomari Kapombe

Hiyo ni habari njema kwa mashabiki wa Simba kwani Coulibaly huenda akawa njiani kutua Msimbazi.

Ingawa picha hiyo haikuwa na maelezo mengi, ni dhahiri uongozi wa Simba utakuwa umemalizana na mkali huyo.

USAJILI: MAVUGO Kutimkia Zambia

Mshambuliaji wa zamani wa Simba Sc Laudit Mavugo amekamilisha mazungumzo ya awali na klabu ya NAPSA Stars Fc ya Zambia tayari kwa kukipiga nchini humo. .
.
Habari ambazo tumezipata @sokaonlinetz zimesema Mavugo anaweza akasaini mkataba na klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu nchini Zambia muda wowote kuanzia sasa #sokaonlineUpdates

USAJILI: Yanga mbioni Kumnasa mchezaji Huyu

Uongozi wa klabu ya Yanga uko mbioni kumalizana na Lipuli Fc ili kukamilisha usajili wa nahodha wa timu hiyo ambaye ni mlinzi anayemudu nafasi za beki wa kati na pembeni, Ally Sonso.

Sonso amekuwa katika kiwango bora msimu huu akiwa miongoni mwa wachezaji walioitwa na Emmanuel Amunike kuunda kikosi cha timu ya Taifa mwezi uliopita.

Sonso amethiboitisha kumalizana na Yanga akiwa tayari kuelekea Jangwani lakini akisubiri viongozi wa Lipuli Fc wamalizane na wenzao wa Yanga.

Sonso anakuwa mchezaji wa pili kuwaniwa na Yanga katika kipindi cha miezi sita baada ya mabingwa hao wa kihistoiria kumkosa Adam Salamba aliyetua Simba mwishoni mwa msimu uliopita.