Timu Zinazotaka Wachezaji wa SIMBA Zapewa Mashari

Simba haina shida wachezaji kuwatoa kwa mkopo wale ambao hawapati nafasi kwenye kikosi chao lakini timu ambayo inahitaji huduma ya wachezaji hao basi wanapaswa kujipanga kupangua masharti mawili magumu ukiachana na yale madogo madogo.

Sharti la kwanza ambalo limewekwa ni kuhakikisha huko watakakokwenda wanacheza kikosi cha kwanza na sio kukaa benchi ama jukwaani.

Sharti la pili ni kuhakikisha wanawapa huduma zote kwa jinsi watakavyokubaliana ikiwemo, mshahara, posho kuishi maisha mazuri yasiyokuwa ya mawazo hasa suala la kukosa mshahara kwa zaidi ya mwezi.

Kwasasa viongozi wa Simba wanasubiri ripoti ya kocha mkuu Patrick Aussems ili kuona ni wachezaji gani amependekeza waondolewe kwa mkopo na kama atahitaji kuongeza wachezaji na kwa nafasi gani.

Kuna taarifa kwmaba nyota watatu wa Simba Mohamed Rashid ‘Mo Rashid’, Marcel Kaheza na kipa Mohamed Said ‘Nduda’ watatolewa kwa mkopo katika timu ambazo zitahitaji huduma zao na kukubali masharti hayo huku kipa Emmanuel Mseja yeye anasubiri barua pekee ingawa yupo kwenye mazungumzo ya chini chini na Caostal Union ya Tanga.

Aliyekuwa Kaimu Rais wa Simba ambaye sasa ni mmoja wa wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi, Salim Abdallah ‘Try Again’ ambaye ameombwa kuendelea na majukumu yake hadi hapo baadaye Bodi itakapoanza majukumu yake rasmi alisema wamepokea maombi ya timu nyingi zikomba huduma za wachezaji wao.

Try Again amesema kuwa wana maombi mengi lakini hadi sasa hakuna maombi yaliyofanyiwa kazi kwani wanasubiri kocha wao atoe mapendekezo kupitia ripoti yao ila tayari wameweka masharti yao ambapo atakayevuka hayo atapewa mchezaji kama itatokea amependekezwa na kocha.

Simba imepokea maombi mengi ya mshambuliaji wao Mo Rashid ambapo timu tano zimetuma barua ambazo ni Singida United, Lipuli FC, Prisons, Coastal Union na KMC huku Kaheza anasakwa na timu mbili KMC na Alliance upande wa Nduda bado hakuna timu iliyojitokeza hadi sasa.

Try Again alisema, “Mo Rashid anatafutwa na timu nyingi sana na huenda tukaendelea kupokea maombi, ila hatuwezi kuamua lolote hadi hapo tutakapopata ripoti kutoka kwa kocha mkuu maana kila kitu tumemwachia akifanye yeye.

“Pia hizi timu zinazohitaji wachezaji wetu kiukweli wakubaliane na baadhi ya haya mammbo, apate nafasi ya kucheza kwani hiyo ndiyo maana halisi ya kupelekwa kwa mkopo kwani mchezaji akitolewa kwa mkopo matarajio ni kumrejesha tena kikosi kwetu wakati yupo kwenye kiwango kizuri zaidi.

“Timu hizo zitambue kwamba mchezaji tutakayewapa basi apate huduma zote, asiwe na njaa kabisa ya mshahara na mambo mengine ambayo yanaweza kuchangia kiwango chake kishuke, wamlee kama tunavyowalea sisi wachezaji wetu, vinginevyo itakuwa vigumu kuwapata wachezaji hao kutoka kwetu,” alisema Try Again.

Try Again alifafanua pia kuwa masuala yote ya ufundi yameachwa kwa Aussems ikiwemo kocha msaidizi na mapendekezo mengine ya usajili na mashindano yote ya ndani na nje ya nchi kwamba mahitaji atakayohitaji viongozi watakuwa watekelezaji.

“Kila kitu kipo chini ya kocha mkuu, hatutaki kumwingilia, hivyo akisema anahitaji kocha msaidizi na akimpendekeza basi sisi tutafanya utekelezaji ikiwemo mambo mengine, hivyo kwasasa tunamsubiri yeye tu,” alisema Try Again.

Aussems yeye alisema ataandaa majina ya wachezaji watano hadi sita atakaowasajili ila kati ya hao mchezaji mmoja tu ndiye atapendekeza asajiliwe wakati huu wa dirisha dogo na kufafanua kwamba, “Kati ya hao napendekeza straika mmoja tu mwenye uwezo wa kufunga na kutengeneza nafasi kwa wenzake,”.

Mpaka sasa kuna majina ya wachezaji wanaotajwa kwenye usajili wa Mabingwa hao watetezi wa ligi kuu Bara akiwemo Francis Kahata kutoka Gor Mahia ingawa ana mkataba na timu yake, Epharaim Guikan na Philomeno Otieno wote wa Gor Mahia pamoja na Sadam Juma wa KCCA ya Uganda.

Mwanaspoti

Usajili: Simba sc Yakanusha Kuhusu Niyonzima kusajiliwa AZAM

Afisa Habari wa Simba Haji Manara amemshukia mwandishi na mchambuzi wa soka nchini Shaffih Dauda baada ya kuweka taarifa kwenye ukurasa wake wa matandao kijamii kuwa kiungo Haruna Niyonzima yuko mbioni kusajiliwa na Azam Fc.

Manara ameshangazwa na taarifa hizo alizodai ni za kiuchonganishi.

“Tunajua Shaffih unatumika na Maadui wa Simba kutaka kutuvuruga kusudi ili kubalance na sisi tuonekane tuna mgogoro na wachezaji wetu,” ameandika Manara.

“Haruna Niyonzima yupo kambini na leo atacheza ikimpendeza kocha dhidhi ya Bata Bullets.

“Hivi mtu muungwana kabisa unawezaje kuandika uongo na kufikia kumvalisha jezi ya timu nyingine mchezaji aliye na mkataba na klabu yetu kama si uchochezi na uhuni wa kishamba?,” amehojia Manara

USAJILI: Polisi Tanzania kumnyemelea MHILU

Klabu ya Polisi Tanzania inayoshiriki ligi daraja la kwanza imetuma maombi kwa Yanga kuwataka kwa mkopo wachezaji wawili Yusufu Mhilu na Baruani Akilimali imefahamika.

Maneja wa Polisi, Nelson Ngonyani amethibitisha timu yake kuwataka wachezaji hao ambao wamekuwa na wakati mgumu kupata nafasi kwenye kikosi cha Mwinyi Zahera

Yanga ilishaweka wazi kuwa inakusudia kuwatoa kwa mkopo baadhi ya wachezaji wake chipukizi ambao wamekosa nafasi

Mbali na wachezaji hao, wengine ambao wamekuwa hawapati nafasi na wanaweza wakatolewa kwa mkopo ni pamoja na Ramadhani Kabwili, Emmanuel Martin, Pius Buswita na Yohana Mkomola

Simba sc Kumsajili kiungo huyu Rayon Sport

#TetesiZaUsajili Imeripotiwa kuwa klabu ya Simba Sc tayari imeanza mazungumzo na mshambuliaji wa Rayon Sports Bonfils Caleb Bimenyimana (20) ili kumsajili katika kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili.
Caleb ni moja ya washambuliaji hatari katika kikosi hicho chenye maskani yake nchini Rwanda ambapo alishwahi kuifunga Yanga Sc bao safi katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika msimu uliopita.
#sokaonlineUpdates

USAJILI: Dirisha Dogo kufunguliwa Alhamis hii

Alhamisi, November 15 2018 keshokutwa ndio siku ambayo dirisha dogo la usajili linatarajiwa kufunguliwa.

Vilabu vinavyoshiriki ligi kuu ya Tanzania Bara vitakuwa na nafasi ya kuboresha vikosi vyao ili kuhakikisha vinafanya vizuri msimu huu.

Yanga ni miongoni mwa timu ambazo zinalazimika kulitumia vyema dirisha hilo ili kurekebisha mapungufu yaliyoonekana na benchi la ufundi.

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera alisema timu yake inahitaki kusajili wachezaji wanne wanaocheza nafasi za beki, kiungo, winga na mshambuliaji.

Zahera ambaye yuko DR Congo kwa majukumu ya timu ya Taifa alisema tayari amewaachia viongozi wa Yanga kazi ya kukamilisha usajili wa wachezaji hao.

Juzi Mwenyekiti wa Kamati ya usajili ya Yanga Hussein Nyika alisema wamekusudia kukamilisha usajili wa wachezaji wote waliopendekezwa na kocha Zahera.

Zahera aliyefanikiwa kuiongoza Yanga kucheza zaidi ya miezi mitatu bila ya kufungwa amesema kama wachezaji hao watapatikana, timu hiyo itakuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kurejesha ubingwa wake uliokwenda Msimbazi msimu uliopita.

Wengi wamekuwa wakijiuliza Yanga ina pesa za kukamilisha usajili huo?

Nyika hakuwa tayari kulizungumzia hilo lakini amesisitiza anachojua yeye ni kuwa watawasajili wachezaji waliopendekezwa na Zahera.

Singida United Yajitosa kumwania KAHEZA, RASHID Simba sc

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems ametoa ruhusa kwa wachezaji wake wawili, Marcel Kaheza na Mohammed Rashid kutolewa kwa mkopo dirisha dogo la usajili litakapofunguliwa mwishoni mwa wiki hii.

Wachezaji hao wamekuwa hawapati nafasi ya kucheza kwenye kikosi cha Simba kutokana na uwepo wa ushindani mkali wa namba unaosababishwa na ubora wa wachezaji kikosini.

Klabu ya Singida Unuted imeonyesha nia ya kutaka kuwachukua wachezaji wote wawili ili kuongeza nguvu kwenye kikosi chao ambacho kimekimbiwa na wachezaji wengi kutokana na ‘ukata’

Tanzania Prisons ilikuwa timu ya kwanza kujitokeza ikimtaka mshambuliaji wao wa zamani Mo Rashidi aliyeifungia timu hiyo mabao 10 msimu uliopita

Simba imedhamiria kuimarisha kikosi chake wakati wa dirisha dogo la usajili huku ikipanga kuwatoa kwa mkopo baadhi ya wachezaji waliokosa namba ili kulinda viwango vyao

Simba Sc: Kumsajili Thomas ULIMWENGU

#TetesiZaUsajili Imeripotiwa kuwa klabu ya Simba Sc ipo kwenye mchakato mzito kuhakikisha inamsajili nyota wa zamani wa Tp Mazembe Thomas Ulimwengu (25) kuelekea kwenye dirisha dogo la usajili litakalofunguliwa mapema wiki ijayo November 15.

Habari za chini chini zilizotufikia zimedai tayari uongozi wa klabu hiyo umepanga mkakati wa kuanza kuzungumza nae wiki hii ili kupata saini yake mara baada ya kuvunja mkataba na klabu yake ya Al Hilal ya Sudan

Ikumbukwe kabla ya kutua Al Hilal ziliwahi kuzagaa taarifa kuwa nyota huyo angesajiliwa Yanga kutokana na uongozi wa klabu hiyo kuonyesha nia ya kumhitaji #soka Updates

SIMBA SC: Kuwatoa watatu kwa Mkopo

Kuelekea dirisha dogo la usajili ambalo litafunguliwa wiki ijayo Novemba 15 mastaa watatu wa Simba wamekubali yaishe na muda wowote kuanzia sasa watatolewa kwa mkopo kwenda kuzitumikia klabu nyingine.

Nyota hao ni Mohammed Rashid, ambaye alisajiliwa na Simba msimu huu akitokea klabu ya Tanzania Prison ambapo msimu uliopita alimaliza ligi akiwa amefungia mabao kumi.

Tangu ametua Simba Rashid hajacheza hata mechi moja ya ligi ingawa alianza vizuri kwa kuonesha kiwango katika mashindano ya SportPesa na Kagame Cup, ambapo alifunga bao katika hatua ya makundi.

Marcel Kaheza, ambaye alisajiliwa na Simba mwanzo wa msimu akitokea Majimaji huku alikuwa nyota baada ya kumaliza msimu akiifungia timu yake mabao 12 licha ya kwamba timu hiyo ilishuka daraja.

Said Mohammed ‘Nduda’ naye ni miongoni mwa nyota ambao watatolewa kwa mkopo na kinachosubiliwa ni muda kufika ili kulitimiza hilo kwani, msimu mmoja na nusu aliokuwa katika kikosi cha Simba amecheza mechi moja tu dhidi ya Kagera Sugar msimu uliopita.

Rashid alisema tayari nimekubaliana na kocha kwamba nikatafute nafasi ya kucheza kutokana na ambao nacheza nao hapa katika nafasi moja watanipa muda mdogo wa kucheza.

“Nimekubaliana naye na ameniambia kama nitafanya vizuri huko ambapo nitakwenda nafasi ya kurudi hapa ipo wazi,” alisema Rashid ambaye anawindwa na Alliance, Mwadui, Prison na KMC ambao wanapewa nafasi kubwa ya kumnasa nyota huyo.

Kocha wa Simba Patrick Aussems alisema katika kikosi chake nyota wote wanauwezo ila wale ambao hawajapata nafasi ya kutumika ni kutokana na changamoto ya kuwania nafasi ya kucheza.

“Changamoto ya kuwania nafasi ya kucheza ni kubwa mno katika timu yangu na haswa wale wachezaji ambao, wanapata nafasi ya kucheza kama wapo tayari nitawaruhusu lakini kama watafanya vizuri nafasi ya kurudi ipo wazi,” alisema Aussems.

Mwanaspoti

CHIRWA: Akaribia Kutua Azam Fc

Imeripotiwa kuwa mshambuliaji wa zamani wa Yanga Obrey Chirwa anaelekea klabu ya Azam Fc baada ya kuwekewa ngumu na kocha wa Yanga Mwinyi Zahera.

Mshambuliaji huyo inaelezwa atasaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Azam wiki ijayo dirisha la usajili litakapofunguliwa.

Chirwa alikuja nchini kwa mwaliko wa Yanga akitokea nchini Misri baada ya kuvunja mkataba wake katika klabu ya Nogoom El Mostakbal FC inayoshiriki ligi daraja la pili.

Inadaiwa Yanga imekamilisha mazungumzo na mshambuliaji kutoka nchini Ghana ambaye ni mmoja wa wachezaji wanne waliotajwa na kocha Zahera kuwa wanaweza kutua Yanga wakati wa dirisha dogo la usajili linalofunguliwa Alhamisi ijayo

Kutokana na wasiwasi ulioonyeshwa na kocha Zahera juu ya tabia ya Chirwa, inaelezwa uongozi wa Yanga umeamua kuachana nae.

Azam Fc ilikuwa ikihusishwa na Chirwa hata kabla hajatimkia nchini Misri.

Kocha Mkuu wa timu hiyo Hans van Pluijm ambaye ndiye aliyemleta Chirwa Tanzania wakati akiinoa Yanga, amependekeza mshambuliaji huyo asajiliwe na Azam.

Chirwa sasa atakwenda kuungana na mshambuliaji mwingine aliyetokea Yanga Donald Ngoma ambaye amepona majeraha yake na tayari ameifungia timu hiyo mabao matatu kwenye ligi