
Huo utakuwa mchezo wa 19 kwa timu hizo kukutana kwenye ligi katika kipindi cha miaka 10
Katika michezo 18 iliyopita, Yanga na Azam Fc zimekuwa na matokeo sawa ambapo Yanga imeshinda michezo sita, Azam Fc ikishinda sita pia huku zikitoka sare mara sita
Hizi hapa takwimu za matokeo ya michezo iliyopita;
2008/09
Azam 1-3 Yanga (Oktoba 15, 2008)
Yanga 2-3 Azam (Aprili 8, 2009)
2009/10
Azam 1-1 Yanga (Oktoba 17, 2009)
Yanga 2-1 Azam (Machi 7,2010)
2010/11
Azam 0-0 (Okt 24, 2010)
Yanga 2-1 Azam (Machi 30, 2011)
2011/12
Azam 1-0 Yanga (Sept 18, 2011)
Yanga 1-3 Azam (Machi 10, 2012)
2012/13
Azam 0-2 Yanga (Nov 4, 2012)
Yanga 1-0 Azam (Feb 23, 2013)
2013/14
Azam 3-2 Yanga (Sept 22, 2013)
Yanga 1-1 Azam (Machi 19, 2014)
2014/15
Yanga 2-2 Azam (Des 28, 2014)
Azam 2-1 Yanga (Mei 5, 2015)
2015/16
Yanga 1-1 Azam (Okt 17,2015)
Azam 2-2 Yanga (Machi 5, 2016)
2017/2018
Azam fc 1-2 Yanga sc (Junuari 27/1/2017
Yanga 1-3 Azam Fc (May 28/5/2018
Katika kipindi cha misimu mitatu iliyopita, upinzani wa Yanga na Azam Fc umekuwa ukiongezeka hasa baada ya Azam Fc kuanza utamaduni wa kusajili wachezaji kutoka Yanga
Baada ya Azam Fc kuwasajili Didier Kavumbagu na Frank Domayo, mwaka juzi Yanga ilimnyakua Gadiel Michael
Mwaka jana Azam Fc iliwasajili Donald Ngoma aliyeachwa na Yanga na baadae Obrey Chirwa
Ngoma na Chirwa wanatarajiwa kuongoza safu ya ushambuliaji ya Azam Fc kwa mara ya kwanza kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Yanga
Chirwa aliifunga Yanga mapema mwaka huu kwenye michuano ya kombe la Mapinduzi katika mchezo ambao Azam Fc ilishinda mabao 3-0
Hata hivyo Yanga haikupeleka kikosi chake cha kwanza katika michuano hiyo ambayo Azam Fc iliibuka mabingwa
Ni mchezo ambao Yanga inahitaji kupata ushindi ili kuweka hai matumaini ya kutwaa ubingwa huku pia ikiiombea Simba iendelee kupunguzwa kasi katika michezo yake ya viporo
Matokeo tofauti na ushindi kwa Yanga huenda yakafifisha nafasi ya kutwaa ubingwa kwa vinara hao wa ligi kuu msimu huu
Azam Fc haina cha kupoteza kwani tayari imeshajiondoa katika kinyan’ganyiro cha kuwania ubingwa ikiweka mkazo zaidi kwenye michuano ya kombe la FA (ASFC)
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema mchezo huo hautakuwa mwepesi kutokana na ubora wa kikosi cha Azam Fc hata hivyo ni matokeo ya ushindi pekee ambayo yanaweza kuwapa nafasi ya kuwa mabingwa
“Hii ni mechi ngumu kwetu, Azam Fc ni timu nzuri ambayo ina ushindani wa hali ya juu. Tunafanya maandalizi maalum ili tuweze kuwafunga,naamini tukishinda tutajiweka katika mazingira mazuri zaidi ya kuchukua ubingwa,” amesema
Yanga inaongoza ligi ikiwa na alama 74, ikiwa mbele ya Azam Fc inayoshika nafasi ya pili kwa tofauti ya alama nane

















