
Mchezo unatarajiwa kuanza saa kumi kamili jioni
Yanga iliyojikusanyia alama 74, iko mbele ya Azam Fc kwa tofauti ya alama nane, inahitaji ushindi katika mchezo huo ili kuendelea kuweka hai mbio za kuwania ubingwa msimu huu
Hata hivyo, mchezo hautakuwa mwepesi kutokana na uimara wa kikosi cha Azam ambacho tangu kimtimue kocha Hans van Pluijm kimepoteza mchezo mmoja tu
Kocha Mwinyi Zahera amesema amewaandaa wachezaji wake kikamilifu lengo lao likiwa kushinda
Amesema ni mchezo ambao wanahitaji kupambana na kuwa makini zaidi, hawapaswi kufanya makosa mengi na lazima watumie nafasi
Timu zote zitawakosa wachezaji wake waandamizi Kelvin Yondani na Aggrey Morris wanaotumikia adhabu ya kukosa michezo mitatu





























