Francis Kahata amegoma kuongeza mkataba katika klabu hiyo huku akihusishwa kusajiliwa na Simba mkataba wake utakapomalizika mwezi wa saba

Kiungo fundi wa Gor Mahia Francis Kahata amegoma kuongeza mkataba katika klabu hiyo huku akihusishwa kusajiliwa na Simba mkataba wake utakapomalizika mwezi wa saba

Msimu huu Kahata ameisaidia Gor Mahia kutwaa taji la ligi kuu ya Kenya pamoja na kuisaidia timu hiyo kufika hatua ya robo fainali kombe la Shirikisho Barani Afrika

Hata hivyo fundi huyo wa mpira anataka kuungana na Meddie Kagere mshambuliaji wa zamani wa Gor Mahia ambaye kwa sasa yuko Simba

Inaelezwa Kagere amemshawishi kiungo huyo ambaye walicheza nae katika klabu ya Gor Mahia

Gor Mahia inakabiliwa na hali ngumu ya kiuchumi na huenda ikawapoteza nyota wake muhimu wanaowania na timu kadhaa

Mshambuliaji tegemeo wa timu hiyo Jacques Tuyisenge yuko mbioni kukamilisha usajili kunako klabu ya Atletico De Luanda ya nchini Msumbiji

Baada ya kumkosa msimu uliopita, Simba ina nafasi nzuri ya kumsajili Kahata msimu huu

BOCCO Ataka Shangwe za Ubingwa zihamie Morogoro

Jana mashabiki wa Simba waliojitokeza uwanja wa Taifa kushuhudia ‘mnyama’ akikabidhiwa kombe baada ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu, hawakufurahia kuahirishwa kwa hafla hiyo

Licha ya mvua kunyesha, baadhi ya mashabiki walikubali ‘kulowana’ ili mradi tu washuhudie tukio hilo la kihistoria

Hata hivyo Bodi ya ligi iliahirisha hafla hiyo baada ya mgeni rasmi, Waziri wa Mambo ya Ndani Mh Kangi Lugola kupata udhuru

Mtendaji wa Bodi ya Ligi Boniface Wambura alisema sherehe hizo zimehamishiwa mkoani Morogoro, zitafanyika baada ya mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa keshokutwa Jumanne katika uwanja wa Jamhuri

Akingumza baada ya mchezo dhidi ya Biashara United uliomalizika kwa sare ya bao 1-1, nahodha wa Simba John Bocco aliwashukuru mashabiki waliojitokeza uwanja wa Taifa kuwaunga mkono licha ya hali ya mvua

Yawezekana na wewe ulikuwa na wasiwasi kuwa Thomas Tuchel angetimuliwa?

Yawezekana na wewe ulikuwa na wasiwasi kuwa Thomas Tuchel angetimuliwa?
:
Hapana. PSG wamemuongezea mkataba mpaka 2021. Licha ya matokeo dhaifu bado wana imani na uwezo wake. Labda nao wamechoshwa na tabia ya kutimua wakufunzi hovyo.
:
💉PSG walipoteza jumla ya mechi 4 ya Ligue 1 kwa misimu miwili 2017 & 2018
💉PSG wamepoteza jumla ya mechi 5 za Ligue 1 ndnai ya msimu mmoja tu 2019
::
✍️Takwimu zake kwa ujumla
– Mechi: 55
– Ushindi: 40
– Vipigo: 9
– Mataji: 2

Magufuli atumia simu ya mkononi kuwapiga picha Kikwete, Rais Ramaphosa

Nchini Afrika Kusini leo Jumamosi Mei 25, 2019 ni siku ya kukumbukwa kutokana na Rais Cyril Ramaphosa kuapishwa kuwa kiongozi wa Taifa hilo kwa muhula wa pili.
Katika hafla ya kuapishwa kwake iliyohudhuriwa na viongozi wa nchini mbalimbali, akiwemo Rais John Magufuli na Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kiwete kuliibuka matukio mengi ya kufurahisha.

Moja kati ya matukio hayo ni kitendo cha Rais Magufuli kutumia simu ya mkononi kuwapiga picha Rais Ramaphosa na Kikwete.

Tukio hilo limevuta hisia za watu wengi katika mitandao ya kijamii na kushangazwa na Rais Magufuli jinsi alivyoshikilia vyema simu hiyo na kuwapiga picha wawili hao.
Viongozi hao walionekana kufurahia tukio hilo wakiwemo baadhi ya marais wa mataifa mengine waliokuwa pembeni yao.
Rais Magufuli ameambatana na Kikwete pamoja na makamu mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula nchini Afrika Kusini kuhudhuria sherehe hizo.
Ramaphosa ameapishwa na Jaji Mkuu wa Afrika Kusini, Mogoeng Mogoeng.

Hafla hiyo ilipambwa kwa maonyesho ya ndege za kijeshi zilizorushwa angani na askari waliotua kwa miavuli na kupigwa mizinga ya heshima kwa Amiri Jeshi Mkuu huyo.

Wizara ya Maliasili na Utalii imemteua Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta kuwa balozi wa hiari wa utalii.

Wizara ya Maliasili na Utalii imemteua Nahodha wa Taifa
Stars, Mbwana Samatta kuwa balozi wa hiari wa utalii.Katika majukumu yake, Waziri @hkigwangalla amesema,
Samatta atatakiwa kuzungumza Kiswahili mara kwa mara,
kuitaja #Tanzania na pia kutumia bendera ya nchi. . . … .. . . 👉 Samatta ambaye ni mchezaji wa timu ya
KRC Genk ya Ubelgij atashuka nchini
usiku wa saa 9 kwa ajili ya kujiunga na
Timu ya Taifa ambayo inakwenda
kushiki michuano ya Afcon nchini Misri
na inakwenda ikiwa ni baada ya miaka
39 kupita.

FT: Simba 1-1 Biashara United

Mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara kati ya Simba, mabingwa msimu huu na Biashara United umemalizika kwa timu hizo kutoka sare ya kufungana bao 1-1

Mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa Taifa, ulivurugwa na mvua zilizojaza maji katika sehemu ya kuchezea ya dimba la Mkapa

Biashara United ilitangulia kupata bao la kuongoza kupitia kwa Innocent Edwin kwenye dakika ya 14 na Simba ikasawazisha dakika tatu baadae kupitia kwa Clatous Chama

Mashabiki hawakujitokeza kwa wingi uwanjani kutokana na hali ya mvua inayoendelea kunyesha jijini Dar es salaam

Yatibua sherehe za ubingwa

Bodi ya Ligi imelazimika kuahirisha sherehe za kuwakabidhi Simba kombe kutokana na changamoto ya mvua

Aidha Mtendaji wa Bodi Boniface Wambura amesema mgeni Rasmi Mh Kangi Lugola naye alipata dharura

Simba sasa itakabidhiwa ubingwa mkoani Morogoro siku ya Jumanne, itakapochuana na Mtibwa Sugar katika mchezo wa kumaliza msimu

Uongozi wa Simba umewataka mashabiki wa timu hiyo mkoani Morogoro kujiandaa kuipokea timu na kuwa tayari kwa shamrashamra za kihistoria

Nyota wapya yanga wajifua na kikosi cha yanga

Uongozi wa Yanga tayari umewapokea nyota wanne wa kigeni wanaotarajiwa kusajiliwa na timu hiyo kwa ajili ya msimu ujao

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema anatarajia kukamilisha usajili wa nyota sita wa kigeni pamoja na wazawa wawili kabla ya kuondoka kwenda DR Congo kujiunga na kambi ya timu ya Taifa

Nyota wa kigeni waliohudhuria mazoezi ya Yanga jana ni pamoja na kiungo mwenye umri wa miaka 20 raia wa Nigeria Victor Patrick Akpan aliyekuwa akikipiga na JKU ya Zanzibar

Akpan yuko kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Nigeria umri chini ya miaka 23

Wengine ni beki wa kati Mohammed Ali Camara mwenye umri wa miaka 21 kutoka klabu ya Horoya AC ya Guinea.

Camara aliitumikia timu ya Taifa ya Guinea U20 na tayari ameitumikia timu ya wakubwa mara moja

Wengine ni mshambuliaji Shehu Magaji Bulama raia wa Nigeria na kiungo Allex Komenan kutoka nchini Ivory Coast

Bulama na Komenan watafanyiwa majaribio na Zahera kabla kuidhinisha kama wasajiliwe au la