MO DEWJI: Apongeza UBINGWA – SIMBA, Aweka wazi Mipango ya Msimu UJAO

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ amewapongeza wachezaji, viongozi na mashabiki wa timu baada ya kufanikiwa kutwaa ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mo amesema ubingwa huo matokeo ya ushirikiano na umoja ulioonyeshwa na Wanamsimbazi tangu mwanzoni mwa msimu

Aidha Mo amesema shamrashamra za ubingwa zitafanyika May 25 wakati timu hiyo itakabidhiwa kombe katika mchezo dhidi ya Biashara United

Katika hatua nyingine Mo ameipongeza Yanga kwa kuipa changamoto Simba katika mbio za kuwania ubingwa.

Amewapongeza viongozi wapya wa timu hiyo na kuwataka waimarishe timu yao ili iweze kuipa changamoto zaidi Simba kwani anaamini uimara wa timu zote utaongeza ubora wa soka la Tanzania

Aussems kuendelea kuinoa Simba

Mo amesema baada ya kocha Mkuu Patrick Aussems kutimiza masharti yote ya mkataba wake, wanakusudia kumpa mkataba mpya

Mwaka jana Aussems aliposaini mkataba wa mwaka mmoja, alipewa masharti mawili ambapo moja ni kutwaa ubingwa wa ligi kuu na la pili ni kutinga hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Maboresho ya kikosi

Mo amesema Aussems leo atawasilisha ripoti ya maboresho ya Simba kwa ajili ya msimu ujao.

Aussems atapendekeza wachezaji ambao anataka waachwe/watolewe kwa mkopo pia kocha huyo anatakiwa kupendekeza wachezaji ambao anataka wasajiliwe

Mo amesema wamedhamiria kuifanya Simba iwe imara mara dufu ili kuhakikisha inafanya vizuri zaidi kwenye michuano ya CAF msimu ujao

Amesema watashindana na vilabu vikubwa barani Afrika kama Al Ahly, TP Mazembe, Zamalek nk katika kuwania wachezaji wazuri

Kuhusu Kambi

Kama ilivyokuwa msimu uliopita, Mo amesema msimu huu Simba itaweka kambi barani Ulaya katika nchi ya Ureno au nchini Marekani

HIKI HAPA KIKOSI CHA YANGA KITAKACHO CHEZA LEO DHIDI YA MBEYA CITY

1. Klaus Kindoki

2. Haruna Moshi

3. Haji Mwinyi

4. Cleofas Sospeter

5. Kelvin Yondani

6. Feisal Salum

7. Deus Kaseke
8. Gustapha Simon
9. Heritier Makambo

10. Papi Tshishimbi

11. Shabani Mangula
SUB

Ramadhani Kabwili
Jaffar Mohammed
Bakari

Raphael Daudi
Pius Buswita
Matheo Anthony

Amissi Tambwe

HAJI MWINYI: Ajiandaa na Maisha Nje ya YANGA

Beki Haji Mwinyi ni miongoni mwa wachezaji wa Yanga ambao mikataba yao inamalizika baada ya mchezo wa mwisho wa ligi

Beki huyo aliyeitumikia Yanga kwa zaidi ya miaka minne, atakuwa huru baada ya Yanga kuumana na Azam Fc wiki ijayo

Amezikaribisha timu zinazohitaji huduma yake kwa ajili ya msimu ujao

“Mkataba wangu na Yanga unamalizika msimu huu. Baada ya hapo nitakuwa huru”

“Nakaribisha klabu yeyote inayohitaji huduma yangu kwa msimu ujao waje tukae mezani tuzungumze, lakini kuhusiana na ofa nilizonazo mezani hadi sasa siwezi kuweka wazi hadi hapo nitakapomaliza msimu wangu kwa michezo miwili iliyobaki,” Mwinyi aliiambia Mwanaspoti

“Sikuwa na namba kikosi cha kwanza, lakini hiyo haina maana kwamba kiwango changu kimeshuka, nipo vizuri na nina uwezo wa kupambana. Kutokana na uzoefu nilionao na naweza kucheza timu yeyote”

Haji Mwinyi hakuwa na wakati mzuri msimu huu katika kikosi cha Zahera akishindwa kutamba mbele ya Gadiel Michael aliyekuwa chaguo la kwanza

Yanga imepanga kutowaongezea mikataba wachezaji ambao hawakucheza angalau nusu ya michezo ya ligi kuu msimu huu

BOSS – SEVILLA Aipongeza Simba kutwaa UBINGWA

Timu ya Sevilla imewasili nchini usiku wa kuamkia leo tayari kwa mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Simba utakaopigwa kesho Alhamisi, saa moja jioni katika uwanja wa Taifa

Katika Mkutano na Waandishi wa habari leo, Rais wa Sevilla Jose Castro ameeleza kufurahia ujio wao hapa nchini hasa ikizingatiwa wao wanakuwa timu ya kwanza kutoka Hispania kucheza Tanzania

Aidha ameipongeza Simba kwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Tanzania Bara

“Niwapongeze sana Simba ya Tanzania kwa kuchukua ubingwa wa ligi Kuu, tumekuja kucheza na timu bora. Ni heshima sana kuja Tanzania na bila shaka tutakua ni timu ya kwanza ya Laliga kuja Tanzania,” amesema

Wakati Sevilla ikiwa tayari imewasili, wapinzani wao Simba nao watatua leo kutoka mkoani Dodoma baada ya kufanikiwa kutetea ubingwa wa ligi kuu kwa msimu wa pili mfululizo

USAJILI: Klabu ya Raja Casablanca ya Morocco 🇲🇦 Imethibitisha kukamilisha Usajili wa kiungo fundi, Fabrice Luamba Ngoma

OFFICIAL! – Klabu ya Raja Casablanca ya Morocco 🇲🇦 Imethibitisha kukamilisha Usajili wa kiungo fundi, Fabrice Luamba Ngoma kutoka Miamba wa Kinshasa, Klabu ya AS Vita Club 🇨🇩.
.
– Kiungo huyo wa Kimataifa wa DR Congo, amesaini Mkataba wa Miaka Mitatu kuwatumikia Miamba hao Baada ya kudumu Kinshasa kwa Misimu miwili.
#transfers

YANGA DIMBANI LEO KUIVAA MBEYA CITY

Kikosi cha Yanga leo kinashuka uwanja wa Uhuru kuikabili Mbeya City katika mchezo wa ligi kuu raundi ya 37

Baada ya Simba kutwaa ubingwa hapo jana, mchezo huo ni wa kukamilisha ratiba tu ambapo mabingwa hao wa kihistoria watakuwa wakilinda heshima yao

Jana Yanga ilifanya maandalizi ya mwisho kwenye uwanja wa Uhuru
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema lengo lao ni kumaliza ligi kwa kushinda michezo yote miwili iliyobaki
Ushindi katika michezo miwili iliyobaki utawafanya wafikishe alama 89 ambazo hata hivyo tayari zimeshapitwa na Simba yenye alama 91

Lakini pia hata kama Yanga itapoteza michezo yote iliyobaki, itaendelea kubaki nafasi ya pili kwani hakuna timu nyingine inayoweza kufikisha alama hizo
Yanga leo inatarajiwa kuwakosa wachezaji saba ambao wanaugua Malaria

Hata hivyo Zahera amesema wachezaji watakaopata nafasi ya kucheza, anaamini wataweza kuipa timu hiyo ushindi
Baada ya mchezo wa leo, Yanga itashuka tena dimbani wiki ijayo May 28 kumaliza msimu kwa kuumana na Azam FC

ZAHERAC: Amlilia AJIBU Kwenda TP MAZEMBE

Kocha Mkuu wa klabu ya Yanga, Mwinyi Zahera amemwambia nahodha na mshambuliaji wa klabu hiyo Ibrahim Ajibu kufikilia mara mbili kuhusu kuihama klabu hiyo mwisho wa msimu huu. Imeelezwa.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Zahera amedai Ajibu ni kiongozi wa wenzake na hapaswi kuwa na mawazo ya kuondoka Yanga na kuwaacha wenzake.

Mkataba wa Ajibu na Yanga unaisha mwisho wa msimu huu na inadaiwa kuwa atajiunga na klabu ya Simba baada ya mkataba wake kuisha na Yanga.

Taarifa za Ajibu kuondoka Yanga zimeanza muda mrefu uliopita na kuleta sintofahamu kwa wapenzi na mashabiki wa timu hiyo kutokana na namna mwenendo wa klabu ulivyo.

Zahera amemuomba Ajibu afikirie zaidi ya mara moja kuhusiana na kuondoka kwake kwa manufaa ya Yanga maana anaheshimu mchango wake.

AJIBU Kutimkia TP MAZEMBE

TP Mazembe itamsajili kiungo wa Yanga Ibrahim Ajib Migomba akitarajiwa kujiunga na timu hiyo Julai 01 2019

TP Mazembe imeiandikia barua Yanga kuitaarifu juu ya nia ya kutaka kumsajili kiungo huyo.

Mazembe itamsajili Ajib baada ya kumaliza mkataba na Yanga

Aidha TP Mazembe imeiomba Yanga impe ruhusa ya siku tatu wiki hii ili aweze kwenda Congo kukamilisha taratibu za usajili

Hii ni habari njema kwa Ajib ambaye msimu huu umekuwa mzuri sana kwake

Ajib ameifungia Yanga mabao sita na kutengeneza mabao 17 kwenye ligi kuu ya Tanzania Bara inayoelekea ukingoni