SIMBA YAIKUNG’UTA MTIBWA SUGAR BAO 3-0 UWANJA WA UHURU YATINGA KILELENI
Simba yaomba sapoti ya mashabiki mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar

Uongozi wa timu hiyo umewataka mashabiki wajitokeze kwa wingi kuwapa sapoti wachezaji katika mchezo huo ambao matokeo ya ushindi ni muhimu
Msemaji wa Simba Haji Manara amesema wachezaji wameahidi kupambana ili kupata matokeo lakini uwepo wa mashabiki wengi uwanjani itakuwa chachu ya wao kufanya juhudi zaidi
“Twendeni uwanjani kwa wingi kama ilivyo kawaida yetu. Tunahitaji alama nane tu tuweze kutwaa ubingwa, tujitokeze kwa wingi kwani kwa umoja wetu tutashinda”
Mchezo wa leo ni kwanza kwa Simba na Mtibwa Sugar kukutana msimu huu. Mchezo wa pili baina ya timu hizo utapigwa mkoani Morogoro, May 28
HIKI HAPA KIKOSI CHA SIMBA KITAKACHO CHEZA LEO DHIDI YA MTIBWA SUGAR
Yanga kukamilisha ukarabati uwanja wa Kaunda

Makamu Mwenyekiti wa Yanga Fredrick Mwakalebela amesema baada ya msimu kumalizika wataanza ukarabati wa sehemu ya kuchezea ‘pitch’ ya uwanja wa Kaunda ili uweze kutumika msimu ujao
“Kwa sasa tutakarabati sehemu ya kuchezea, ni zoezi ambalo litachukua takribani miezi mitatu,” amesema Mwakalebela
“Lengo letu ni kuhakikisha msimu ujao tunakuwa na uwanja wetu wa mazoezi ili kupunguza gharama”
“Gharama tunazotumia kukodi viwanja ni kubwa, pesa hiyo inaweza kutusaidia katika masuala mengine yakiwemo ya usajili”
Kuhusu adha ya mafuriko Jangwani, Mwakalebela amesema kifusi kilichowekwa mwanzo kimepunguza adha hiyo na wanakusudia kuongeza kifusi kingine kabla ya kuanza mchakato wa kupanda nyasi sehemu ya kuchezea
Kadi za njano zamuumiza Fei Toto

Fei Toto tayari amekosa michezo mitatu ya ligi inayotokana na adhabu za kadi za njano
Kiungo huyo aliyesajiliwa na Yanga akitokea JKU ya Zanzibar, hafurahii kadi hizo kwani zinamharibia jina na kumpa sifa mbaya
Fei Toto amesema anachokifanya uwanjani ni kutimiza wajibu na maelekezo anayopewa na Mwalimu.
Anaamini baadhi ya kadi anastahili lakini yapo matukio ambao anadhani hatendewi haki na waamuzi
Aidha kiungo huyo amesema amekuwa akikamiwa na wachezaji wa timu pinzani hali inayomfanya acheze kwa presha kubwa
“Baadhi ya mechi huwa nakamiwa, na kunifanya nicheze kwa presha kubwa. Siwezi kusema uwezo wangu ndio chanzo cha kukamiwa kwani naamini kila timu inaingia uwanjani ikiwa na lengo la kupata alama tatu,” amesema
Zahera aenda Congo, kuiwahi Mbeya City

Zahera anatarajiwa kurudi May 19 siku tatu kabla ya mchezo wa raundi ya 37 ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Mbeya City
Mcongomani huyo amemuachia majukumu kocha Msaidizi Noel Mwandila
Simba yapania kuweka sawa hesabu za ubingwa leo
Baada ya kukosa ushindi katika michezo miwili iliyopita, Simba leo inahitaji ushindi ili kuweka sawa hesabu za ubingwa
Simba inahitaji alama saba kutoka michezo mitano iliyobaki kuweza kutetea ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo
Kama itashinda leo, halafu ikashinda mchezo dhidi ya Ndanda Jumapili, sare au matokeo ya ushindi mchezo dhidi ya Singida United, yatatosha kuipa Simba ubingwa wa pili mfululizo
Meneja wa Simba Patrick Rweyemamu amesema wachezaji wa timu hiyo wako katika hali nzuri kuelekea mchezo huo ambao wamepania kuondoka na alama zote tatu
Magazeti ya leo, Alhamisi, May 16 2019
Yanga kuunda Kamati ya Usajili

Akizungumza na waandishi wa habari leo katika Mkutano uliofanyika Makao Makuu ya Yanga jijini Dar es salaam, Mwenyekiti wa timu hiyo Dk Mshindo Msolla amesema tayari uteuzi umeshafanyika kwa sasa wanafanya majadiliano na wajumbe walioteuliwa kabla ya kuwaweka hadharani
“Wajumbe wa Kamati hiyo tumeshawateua lakini hatuwezi kuwatangaza kabla nao hawajaridhia,” amesema Dk Msolla
“Wiki ijayo tutakuwa na kikao na benchi la Ufundi, pengine katika kikao hicho tutaitangaza Kamati”
“Msimu huu tumedhamiria kufanya usajili makini wenye tija”
Aidha Dk Msolla amesema hata hivyo jukumu la kutafuta wachezaji litabaki kwa kocha Zahera na benchi lake la ufundi, Kamati hiyo itakuwa na jukumu la kumsaidia kukamilisha michakato ya usajili baada ya makubaliano kufikiwa
Dk Msolla amesema kuanzia msimu ujao watawatumia wachezaji waliocheza Yanga zamani kutafuta wachezaji
“Msimu ujao kazi kubwa itafanywa na wachezaji wetu wa zamani kwani tutawapa jukumu la kutembea mikoani kutafuta wachezaji wenye vipaji”





























