
MATOKEO YA MECHI ZA LEO
FT: Mbeya City 1-2 Simba SC (Naldo 22’ : Mkude 68’, Kagere 85’)
.
.
FT: Singida United 1-1 Mtibwa Sugar (Habib Kyombo 32’ : Ismail Aidan 45’+1)
.
.
FT: Ruvu Shooting 3-1 JKT Tanzania (Musa Said 48’, Emmanuel Martin 59’, Fully Maganga 79’: Ally Bilaly 44’)
.
.
FT: Alliance FC 2-2 Kagera Sugar (Birimana Blaise 39’, Dickson Ambundo 90’+5 : Ramadhan Kapera 53’, Peter Mwalyanzi 71’)
.
.
#TanzaniaPremierLeague
Uongozi wa Yanga, wanachama na mashabiki wamepokea kwa masikitiko makubwa sana kifo cha aliekuwa Mwenyekiti mtendaji wa makampuni ya IPP Dkt Reginald A Mengi kilichotokea jana uko falme za kiarabu
Mzee Mengi alikuwa mwanachama na pia mwanafamilia wa Yanga na tunatambua sana mchango wake kwenye klabu yetu
Tunaungana na Familia pamoja na wa Tanzania wote kwenye kipindi hiki kigumu cha Maombolezo
Bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Mchungahella amesema baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kufuta shauri hilo, uchaguzi utafanyika May 05 kama ulivyopangwa
Aidha amesema mpaka sasa zoezi la kampeni linaendelea vizuri na hakuna malalamiko yoyote ya uvunjwaji wa sheria
Mchungahella amesema wanachama wote wenye kadi za zamani (kitabu) na za ki-elektroniki (posta) wataruhusiwa kushiriki katika mchakato huo
Muhimu ni Mwanachama lazima awe amelipia ada ya mwaka

Mchezo huo utapigwa Jumatatu, May 06 katika uwanja wa Samora
Yondani amemaliza kutumikia adhabu ya kukosa michezo mitatu baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar uliopigwa jijini Mwanza
Amekosa michezo dhidi ya Mtibwa Sugar, Azam Fc na Tanzania Prisons
Wachezaji waliojumuishwa kwenye msafara huo ni pamoja na Klaus Kindoki, Ramadhan Kabwili, Kelvin Yondan, Haji Mwinyi, Juma Abdul, Paul Godfrey, Abdallah Shaibu, Endrew Vicent, Said Makapu, Feisal Salum, Mohammed Issa, Papy Tshishimbi, Thaban Kamusoko, Deus Kaseke, Mrisho Ngasa, Ibrahim Ajib, Raphael Daud, Herieter Makambo, Amiss Tambwe, Haruna Moshi, Jaffar Mohamed, Ibrahim Hamid na Pius Buswita
Mchezo wa kwanza wa nusu fainali kombe la FA unapigwa leo kati ya Azam Fc dhidi ya KMC, saa moja jioni uwanja wa Azam Complex
Hafla hiyo ambayo itatumika ‘kuijaza Yanga mapesa’, itawashirikisha wadau wake mbalimbali ambao kwa umoja wao wamedhamiria kuirejesha heshima ya timu hiyo
Mwanamuziki Ali Kiba ni miongoni mwa watu maarufu watakaohudhuria hafla hiyo itakayofanyika Hoteli ya Serena kuanzia saa 12 jioni
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Mh Jokate Mwegelo, Wema Sepetu, Jackline Wolper, Batuli, Vicent Kigosi na Steve Nyerere nao watakuwepo







Mabao mawili yaliyoiwezesha Simba kupata ushindi wa 2-1 dhidi ya Mbeya City leo, yameifanya timu hiyo iwe imefunga mabao 60
Meddie Kagere sasa ndiye kinara wa kuzifumania nyavu akiwa ametupia kambani mabao 17 akiwaacha washindani wake Salum Aiyee (16) na Heritier Makambo (16)
Katika mabao 60 yaliyofungwa mpaka sasa, Kagere, Okwi na Bocco wamechangia mabao 41
Kagere (17), Okwi (10) na Bocco (14)
Lakini pia Simba ndio timu iliyoruhusu mabao machache zaidi mpaka sasa ikiwa imefungwa mabao 12 tu. Azam Fc inafuatia ikiwa imeruhusu mabao 19
Simba inakaribia kutetea ubingwa wake ikihitaji kushinda michezo sita kati ya tisa iliyobaki
Baada ya mchezo dhidi ya Tanzania Prisons keshokutwa, Simba itarejea jijini Dar es salaam ambako itacheza michezo sita katika dimba la Taifa/Uhuru
Huenda ikatangaza ubingwa kupitia michezo hiyo
Tayari vikosi vimeshaingia uwanja, mchezo ukitarajiwa kuanza punde


Mchezo huo uliathiriwa na mazingira ya uwanja uliojaa maji baada ya mvua kunyesha muda mchache kabla ya mchezo kuanza
Mbeya City ilitangulia kufunga bao katika dakika ya 22 kupitia kwa Iddi Selemani Naddo
Hata hivyo Simba ilirejea ikiwa imara kwenye kipindi cha pili na kusawazisha bao hilo kupitia kwa Jonas Mkude kwenye dakika ya 68 kabla Meddie Kagere hajaihakikishia Simba alama tatu muhimu kwa kufunga bao la ushindi kwenye dakika ya 85

Ushindi huo umeifanya Simba ifikishe alama 75, ikiendelea kushika nafasi ya pili kwa tofauti ya alama tano dhidi ya Yanga
Itacheza mchezo mwingine dhidi ya Tanzania Prisons keshokutwa Jumapili hapohapo dimba la Sokoine

