MATOKEO MECHI ZA LEO LIGI KUU

MATOKEO YA MECHI ZA LEO

FT: Mbeya City 1-2 Simba SC (Naldo 22’ : Mkude 68’, Kagere 85’)
.
.
FT: Singida United 1-1 Mtibwa Sugar (Habib Kyombo 32’ : Ismail Aidan 45’+1)
.
.
FT: Ruvu Shooting 3-1 JKT Tanzania (Musa Said 48’, Emmanuel Martin 59’, Fully Maganga 79’: Ally Bilaly 44’)
.
.
FT: Alliance FC 2-2 Kagera Sugar (Birimana Blaise 39’, Dickson Ambundo 90’+5 : Ramadhan Kapera 53’, Peter Mwalyanzi 71’)
.
.
#TanzaniaPremierLeague

Yanga yaomboleza kifo cha Mwanachama wake Dk Mengi

TAARIFA

Uongozi wa Yanga, wanachama na mashabiki wamepokea kwa masikitiko makubwa sana kifo cha aliekuwa Mwenyekiti mtendaji wa makampuni ya IPP Dkt Reginald A Mengi kilichotokea jana uko falme za kiarabu

Mzee Mengi alikuwa mwanachama na pia mwanafamilia wa Yanga na tunatambua sana mchango wake kwenye klabu yetu

Tunaungana na Familia pamoja na wa Tanzania wote kwenye kipindi hiki kigumu cha Maombolezo

Bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Kesi ya kupinga uchaguzi Yanga yafutwa, kadi zote kutumika

Mwenyekiti wa Kamati ya uchaguzi ya TFF Malangwe Mchungahella ambaye Kamati yake inashirikiana na kamati Maalum ya Uchaguzi ya Yanga, amesema kesi iliyokuwa imefunguliwa na Wanachama wawili ya kupinga uchaguzi wa Yanga, imefutwa.

Mchungahella amesema baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kufuta shauri hilo, uchaguzi utafanyika May 05 kama ulivyopangwa

Aidha amesema mpaka sasa zoezi la kampeni linaendelea vizuri na hakuna malalamiko yoyote ya uvunjwaji wa sheria

Mchungahella amesema wanachama wote wenye kadi za zamani (kitabu) na za ki-elektroniki (posta) wataruhusiwa kushiriki katika mchakato huo

Muhimu ni Mwanachama lazima awe amelipia ada ya mwaka

Yondani aongeza nguvu Yanga

Beki kisiki wa Yanga Kelvin Yondani amejumuishwa kwenye kikosi cha timu hiyo kilichoondoka leo kuelekea mkoani Iringa kwa ajili ya mchezo wa nusu fainali kombe la FA dhidi ya Lipuli Fc

Mchezo huo utapigwa Jumatatu, May 06 katika uwanja wa Samora

Yondani amemaliza kutumikia adhabu ya kukosa michezo mitatu baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar uliopigwa jijini Mwanza

Amekosa michezo dhidi ya Mtibwa Sugar, Azam Fc na Tanzania Prisons

Wachezaji waliojumuishwa kwenye msafara huo ni pamoja na Klaus Kindoki, Ramadhan Kabwili, Kelvin Yondan, Haji Mwinyi, Juma Abdul, Paul Godfrey, Abdallah Shaibu, Endrew Vicent, Said Makapu, Feisal Salum, Mohammed Issa, Papy Tshishimbi, Thaban Kamusoko, Deus Kaseke, Mrisho Ngasa, Ibrahim Ajib, Raphael Daud, Herieter Makambo, Amiss Tambwe, Haruna Moshi, Jaffar Mohamed, Ibrahim Hamid na Pius Buswita

Mchezo wa kwanza wa nusu fainali kombe la FA unapigwa leo kati ya Azam Fc dhidi ya KMC, saa moja jioni uwanja wa Azam Complex

Mastaa kibao waalikwa ‘Gala Dinner’ May 11

Siku ya Jumamosi ya May 11 2019 Yanga imepanga kuandika historia jijini Dar es salaam katika hafla maalum ya chakula cha jioni iliyoandaliwa Kamati ya Uhamishaji wa michango inayoongozwa na Mh Anthony Mavunde

Hafla hiyo ambayo itatumika ‘kuijaza Yanga mapesa’, itawashirikisha wadau wake mbalimbali ambao kwa umoja wao wamedhamiria kuirejesha heshima ya timu hiyo

Mwanamuziki Ali Kiba ni miongoni mwa watu maarufu watakaohudhuria hafla hiyo itakayofanyika Hoteli ya Serena kuanzia saa 12 jioni

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Mh Jokate Mwegelo, Wema Sepetu, Jackline Wolper, Batuli, Vicent Kigosi na Steve Nyerere nao watakuwepo

Rekodi ya mabao Simba inatisha

Simba imeendelea ‘kuzikimbiza’ timu nyingine zinazoshiriki ligi kuu ya Tanzania Bara, ikiongoza kwa kufunga mabao

Mabao mawili yaliyoiwezesha Simba kupata ushindi wa 2-1 dhidi ya Mbeya City leo, yameifanya timu hiyo iwe imefunga mabao 60

Meddie Kagere sasa ndiye kinara wa kuzifumania nyavu akiwa ametupia kambani mabao 17 akiwaacha washindani wake Salum Aiyee (16) na Heritier Makambo (16)

Katika mabao 60 yaliyofungwa mpaka sasa, Kagere, Okwi na Bocco wamechangia mabao 41

Kagere (17), Okwi (10) na Bocco (14)

Lakini pia Simba ndio timu iliyoruhusu mabao machache zaidi mpaka sasa ikiwa imefungwa mabao 12 tu. Azam Fc inafuatia ikiwa imeruhusu mabao 19

Simba inakaribia kutetea ubingwa wake ikihitaji kushinda michezo sita kati ya tisa iliyobaki

Baada ya mchezo dhidi ya Tanzania Prisons keshokutwa, Simba itarejea jijini Dar es salaam ambako itacheza michezo sita katika dimba la Taifa/Uhuru

Huenda ikatangaza ubingwa kupitia michezo hiyo

FT : Mbeya City 1-2 Simba

Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba wameendelea kuukaribia ubingwa wa pili mfululizo baada ya leo kuichapa Mbeya City mabao 2-1 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya

Mchezo huo uliathiriwa na mazingira ya uwanja uliojaa maji baada ya mvua kunyesha muda mchache kabla ya mchezo kuanza

Mbeya City ilitangulia kufunga bao katika dakika ya 22 kupitia kwa Iddi Selemani Naddo

Hata hivyo Simba ilirejea ikiwa imara kwenye kipindi cha pili na kusawazisha bao hilo kupitia kwa Jonas Mkude kwenye dakika ya 68 kabla Meddie Kagere hajaihakikishia Simba alama tatu muhimu kwa kufunga bao la ushindi kwenye dakika ya 85

Ushindi huo umeifanya Simba ifikishe alama 75, ikiendelea kushika nafasi ya pili kwa tofauti ya alama tano dhidi ya Yanga

Itacheza mchezo mwingine dhidi ya Tanzania Prisons keshokutwa Jumapili hapohapo dimba la Sokoine