




Simba ilipowasili mkoani Mara jana, shamrashamra za mashabiki zilikuwa kubwa hali hiyo imeendelea mpaka leo ambapo mashabiki walianza kuingia uwanjani tangu saa tatu asubuhi

Mpaka kufika saa 10 jioni huenda mashabiki ambao watachelewa wakalazimika kurudi nyumbani kuushuhudia mchezo huo runingani kwani mpaka sasa uwanja wa Karume unaelekea kujaa
Mashabiki wana shauku ya kuishuhudia Simba ambayo imetua mkoani Mara kwa mara ya kwanza baada ya kupita miaka 15
Baada ya ushindi dhidi ya Alliance na KMC, Simba imeingia Mara ikiwa na shauku yas kupata alama nyingine tatu ili kujisogeza zaidi kileleni mwa msimamo wa ligi
Biashara United imeweka hadharani viingilio vya mchezo huo ambapo VIP ni Tsh 20,000/- Mzunguuko Tsh 5,000/- huku watoto wakiwekewa kiingilio cha Tsh 3,000/-
Mchezo utapigwa kuanzia saa kumi kamili jioni
Kila la kheri mabingwa wa nchi…!
Shirikisho la Soka Barani Ulaya(UEFA) limemfungia mshambuliaji huyo wa Paris Saint-Germain baada ya kuandika maneno ya dharau na kejeli kufuatia timu yake kutolewa na Manchester United katika mchezo wa Klabu Bingwa Ulaya
Mbrazili huyo, aliweka bandiko katika ukurasa wake wa mtandao wa Kijamii wa Instagram lenye kuonesha hasira baada ya Man. Utd kupata penati ndani ya dakika nne za nyongeza wakati shuti lililopigwa na Diogo Dalot lilipomgonga Presnel Kimpembe mkononi
-l
Marcus Rashford alitumia nafasi hiyo aliyopewa na Muamuzi Damir Skomina aliyetoa penati hiyo baada ya kujishauri kutumia mfumo wa uamuzi wa runinga(VAR), kufunga goli na kufanya Manchester United kufuzu kucheza hatua ya robo fainali
Neyma aliandika “Hii ni aibu, wameweka watu wanne wasiojua chochote kuhusu soka kutoa maamuzi baada ya kuangalia marudio ya tukio kupitia VAR. Hakukua na penati. Panawezaje kuwa na penati wakati mpira umempiga mgogoni!” Kisha akatuna

Mchezo huo utapigwa kesho Jumamosi katika uwanja huo
Msafara wa Simba uliwasili mkoani Mara mapema leo na kupokewa na idadi kubwa ya mashabiki waliokuwa na shauku ya kuwaona mabingwa hao wa nchi







Mchezo huo utapigwa kesho Jumamosi, April 27 kwenye uwanja wa Karume
Idadi kubwa ya mashabiki wamejitokeza kwa wingi kuulaki msafara wa mabingwa hao watetezi wakati ukiingia Musoma

Simba tayari imeondoka Mwanza na leo jioni inatarajiwa kujifua kwenye uwanja huo
Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Simba kucheza mkoani Mara baada ya kupita miaka 15
Biashara United inanolewa na beki wa zamani wa Simba Amri Said

Baada ya mchezo dhidi ya KMC jana, mashabiki wa Yanga walionekana kuisemea KMC kuwa imeonewa na waamuzi huku wachezaji wa timu yao wakigoma kufanya mazoezi wakidai mishahara
Tangu jana wachezaji wa Yanga hawafanyi mazoezi wakishinikiza walipwe madai yao ya mishahara ya miezi mitatu huku wengine wakiwa hawajalipwa fedha za usajili mpaka leo
“Badala ya kuhangaika jinsi ya kuwalipa mishahara wachezaji wenu mnahangaika na timu Bingwa inayowafunga kila siku. Kama nyie wananchi wachangieni hao wachezaji walipwe mishahara,” ameandika Manara kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram