Yanga yataka sapoti ya mashabiki mchezo dhidi ya Azam Fc

Mashabiki wa Yanga wameaswa kujitokeza kwa wingi uwanja wa Uhuru kesho kuiunga mkono timu yao ikichuana na Azam Fc

Mratibu wa Yanga Hafidh Saleh amesema wamefanya maandalizi ya kutosha na wana matumaini makubwa ya kupata matokeo mazuri kwenye mchezo huo

“Tunawaomba mashabiki wetu wajitokeze kwa wingi kutuunga mkono. Timu iko tayari kwa ajili ya mchezo huo na lengo letu ni kupata ushindi ambao utaendelea kutuimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi”

Azam Fc itakuwa mwenyeji wa mchezo huo wa kwanza kwa timu hizo kukutana msimu huu

Viingilio kwa majukwaa ya VIP A ni Tsh 15,000/- na VIP B ni Tsh 10,000/- wakati Mzunguuko ikiwa Tsh 5,000/-

Mchezo huo pia utakuwa mbashara kupitia Azam Sport 2 ambapo mtangazaji Baraka Mpenja ndiye atakayeongoza matangazo hayo

Simba yaondoka Mwanza kurejea Dar

Kikosi cha Simba kimeondoka leo jijini Mwanza kurejea jijini Dar es salaam kuendelea na ratiba ya michezo ya ligi kuu ambapo keshokutwa Jumanne itachuana na JKT Tanzania katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Uhuru

Simba imemaliza salama ratiba ya michezo ya kanda ya ziwa ikifanikiwa kushinda michezo mitatu na kufungwa mchezo mmoja

Baada ya mchezo dhidi ya JKT Tanzania, kikosi cha Simba kitaelekea mkoani Mbeya kuzifuata Mbeya City na Tanzania Prisons

Simba yaondoka Mwanza kurejea Dar

Kikosi cha Simba kimeondoka leo jijini Mwanza kurejea jijini Dar es salaam kuendelea na ratiba ya michezo ya ligi kuu ambapo keshokutwa Jumanne itachuana na JKT Tanzania katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Uhuru

Simba imemaliza salama ratiba ya michezo ya kanda ya ziwa ikifanikiwa kushinda michezo mitatu na kufungwa mchezo mmoja

Baada ya mchezo dhidi ya JKT Tanzania, kikosi cha Simba kitaelekea mkoani Mbeya kuzifuata Mbeya City na Tanzania Prisons

Wanaosema Simba ‘inabebwa’ wajitafakari

Afisa Habari wa Simba Haji Manara amewashangaa mashabiki wanaosema klabu hiyo inabebwa na waamuzi wakati timu hiyo imepata mafanikio nje na ndani ya Tanzania kutokana na ubora wa kikosi chake

Manara amesema Simba imekuwa ikicheza kila baada ya siku mbili na inapata matokeo kutokana na ubora wake na si vinginevyo

“Tumefika robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa tulibebwa na nani?” alihoji Manara

“Hata hao Yanga ambao mashabiki wao wanalalamika kuwa tunabebwa nao tuliwafunga, je tulibebwa?”

“Kwa sasa Simba ndio timu yenye kikosi bora Tanzania, ndio mabingwa watetezi na baada ya wiki moja tutakuwa kileleni mwa msimamo wa ligi tayari kurejesha ubingwa Msimbazi”

Simba imebakisha michezo 11, lakini inahitaji kushinda michezo nane tu ili iweze kutwaa ubingwa

Aidha kama Yanga itashindwa kuifunga Azam Fc kesho, Simba itahitaji kushinda michezo miwili tu ili kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi

Aussems ashangazwa na mzuka wa mashabiki Musoma

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amewashukuru mashabiki wa timu hiyo mkoani Mara kwa sapoti waliyotoa kwa mabingwa hao watarajiwa wa ligi kuu kwa msimu wa pili mfululizo

Aussems amesema amefarijika kuona mashabiki wakijitokeza kwa wingi uwanjani jana lakini zaidi juzi Simba ilipotua mkoani Mara

“Tumefarijika na mapokezi waliyotupa mashabiki wa hapa ikiwa ni muda mrefu umepita tangu Simba ije kucheza hapa,” amesema

“Tumewaachia zawadi ya ushindi, sisi tunaelekea Dar ambako tutacheza mchezo mmoja Jumanne (na JKT Tanzania) kisha tutaelekea mkoani Mbeya kuzikabili Mbeya City na Tanzania Prisons”

Msafara wa Simba ulilala jijini Mwanza ambapo leo wanarejea jijini Dar es salaam kwa usafiri wa ndege

Viongozi hakikisheni Yanga inamaliza msimu salama

Mpaka hapa ilipofika Yanga hata kama haitatwaa ubingwa wa ligi kuu, msimu huu utabaki kuwa wa mafanikio kwa mabingwa hao wa kihistoria

Licha ya kukabiliwa na changamoto za kiuchumi, wachezaji wa timu hiyo wamepambana na kuweza kufanya vizuri kwenye ligi huku wakitinga nusu fainali ya michuano ya kombe la Azam (ASFC)

Mwanzoni mwa msimu hakuna aliyeipa Yanga nafasi ya kufanya vizuri kutokana na kushindwa kufanya usajili ‘mkubwa’ ukilinganisha na wapinzani wake Simba na Azam Fc

Bila shaka mgomo waliofanya wachezaji juzi umewasikitisha wengi, ni faraja kusikia uongozi wa timu hiyo umechukua hatua haraka kuirejesha timu katika hali ya kawaida

Wachezaji na benchi la ufundi wamefanya kazi kubwa katika mazingira magumu, litakuwa jambo la kusikitisha kama walichokifanya wakati wa shida kitaharibiwa dakika hizi za majeruhi

Naamini viongozi wameyasikia malalamiko ya wachezaji, wayapatie ufumbuzi mapema ili wamalize msimu kwa moyo mmoja

Yanga bado inawania mataji mawili, wakati huu inapaswa fikra za wachezaji ziwe katika kumaliza msimu kwa nguvu ili washinde angalau taji moja kuliko kufikiria mambo mengine

Niyonzima aomba radhi

Kiungo fundi Haruna Niyonzima amewaomba radhi kwa uongozi wa klabu ya Simba pamoja na mashabiki wa timu hiyo kufuatia kadi nyekundu aliyopewa kwenye mchezo wa jana dhidi ya Biashara United, mchezo ambao Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-0

Niyonzima amesema anajutia tukio alilofanya ambalo lilisababisha apewe kadi nyekundu

“Ulikua mchezo wenye presha kubwa sana ukizingatia tulihitaji sana matokeo kuliko chochote,” amesema

“Iliniumiza sana kutoka uwanjani nikiacha timu yangu pungufu. Niombe radhi kwa klabu yangu mashabiki zetu waliosafiri mpaka Mara na pia wale wote mliokua majumbani mkitizama kupitia televisheni”

“Nilichofanya hakikuwa bora kwa ustawi wa mpira wetu samahani wote mliokwazika, tutapambana mpaka tone la mwisho kwajili ya ubingwa”

Mashabiki wa Simba Mara ‘mmetisha’

Mapokezi na sapoti iliyopata Simba mkoani Mara ni ya kipekee na hakika watu wa Musoma wanastahili pongezi kwa ‘vibe’ la maana waliloonyesha leo

Simba haikuwa imefika Mara katika kipindi cha miaka 15 kutokana na mkoa huo kukosa timu ya ligi kuu, makaribisho iliyopata yanadhihirisha ukubwa wa Simba nchini Tanzania kwa sasa

Baada ya mchezo wa leo kikosi cha Simba kinatarajiwa kuondoka kesho kurejea jijini Dar es salaam kujiandaa na mchezo unaofuata dhidi ya JKT Tanzania

FT : Biashara United 0-2 Simba

Simba imeendeleza umwamba wake kwenye ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya leo kuifumua Biashara United mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Karume, Mara

Simba imefikisha alama 69 sasa ikitofautiana na Yanga kwa tofauti ya alama tano tu huku kibindoni ikiwa na michezo mitano ya viporo

Shukrani za kipekee zimwendee nahodha John Bocco aliyefunga mabao yote mawili kwenye kipindi cha kwanza na kuihakikishia Simba alama tatu muhimu

Bocco amefikisha mabao 14 akichupa mpaka nafasi ya tatu kwenye orodha ya vinara wa mabao nyuma ya Makambo mwenye mabao 15

Aidha Bocco amefikisha idadi ya mabao aliyofunga msimu uiliopita

Katika mchezo huo Simba ilipata pigo baada ya kiungo wake Haruna Niyonzima kutolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumtolea maneno machafu mwamuzi

Simba imemaliza michezo ya kanda ya ziwa na sasa inarejea jijini Dar es salaam ambapo Jumanne itachuana na JKT Tanzania, mchezo utakaopigwa uwanja wa Uhuru