Mratibu wa Yanga Hafidh Saleh amesema wamefanya maandalizi ya kutosha na wana matumaini makubwa ya kupata matokeo mazuri kwenye mchezo huo
“Tunawaomba mashabiki wetu wajitokeze kwa wingi kutuunga mkono. Timu iko tayari kwa ajili ya mchezo huo na lengo letu ni kupata ushindi ambao utaendelea kutuimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi”
Azam Fc itakuwa mwenyeji wa mchezo huo wa kwanza kwa timu hizo kukutana msimu huu
Viingilio kwa majukwaa ya VIP A ni Tsh 15,000/- na VIP B ni Tsh 10,000/- wakati Mzunguuko ikiwa Tsh 5,000/-
Mchezo huo pia utakuwa mbashara kupitia Azam Sport 2 ambapo mtangazaji Baraka Mpenja ndiye atakayeongoza matangazo hayo



























