KELVIN JOHN BADO ANANG’ANG’ANA NA UFUNGAJI BORA AFCON U17

Licha ya kuwepo kwa ushindani mkubwa katika kusaka nafasi ya ufungaji bora wa mashindano ya AFCON U 17 yanayoendelea Nchini, Mshambuliaji wa Serengeti Boys Kelvin John ‘ Mbappe’ amesema mpango wake wa kuibuka kinara wa mabao katika mashindano hayo bado upo pale pale hivyo atahakikisha anapambana ili kutimiza ndoto yake
.
.
Ikumbukwe kuwa Nyota huyo alifunga bao moja katika mchezo wa kwanza wakati Tanzania ikipoteza kwa mabao 4-5 dhidi ya Nigeria huku Edimond John wa Serengeti Boys na Wisdom Ubani wa Nigeria wakifunga mabao mawili kila mmoja na kuongoza katika msimamo wa orodha ya wafungaji.
.
.

Mbali na hilo Kelvin amesema kwasasa wanajipanga kufanya vizuri kuhakikisha wanapata matokeo kwenye mchezo ujao dhidi ya Uganda utakaopigwa Jumatano hii katika uwanja wa Taifa jijini Dar Es Salaam.
.
.
@officialjamesmlaga

TAARIFA MUHIMU. .

Mchezo kati ya Coastal Union dhidi Simba Sc uliotakiwa kuchezwa kesho majira ya saa 10:00 Jioni katika uwanja wa Mkwakwani Tanga, umerudishwa nyuma kwa masaa mawili na sasa utapigwa majira ya saa nane mchana. .
.
Maamuzi hayo yametolewa na shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF ili kuipa nafasi michuano ya vijana AFCON U17 inayoendelea jijini Dar Es Salaam

TAARIFA MUHIMU. .
Mratibu wa klabu ya Yanga Sc Hafidh Saleh amethibitisha kuwa mchezo wao wa kesho dhidi ya Mtibwa Sugar uliotakiwa kupigwa majira ya saa 10 Jioni umerudishwa nyuma kwa masaa mawili na sasa utapigwa majira ya saa 8:00 mchana. .
.
Mchezo huo umerudishwa nyuma ili kupisha mchezo wa AFCON U17 kati ya Serengeti Boys dhidi ya Uganda utakaopigwa majira ya saa 10 Jioni

Mwinyi Zahera ameanza mchakato wa kumsajili mshambuliaji hatari Roderick Mutuma (31)

Kocha Mkuu wa klabu ya Yanga Sc Mwinyi Zahera ameanza mchakato wa kumsajili mshambuliaji hatari Roderick Mutuma (31) raia wa Zimbabwe ambaye kwasasa anakipiga kunako klabu ya Fc Lupopo ya Congo.
.
.
Hata hivyo huenda dili hilo likaota mbawa kutokana na nyota huyo kuwa na mkataba na klabu yake mpaka Disemba 2020 huku thamani yake ikikadiliwa kuwa ni zaidi ya milioni 200.
.
.
Mutuma alijiunga na Fc Lopopo mwishoni mwa mwezi Disemba 2018 kwa mkataba wa miaka miwili akitokea klabu ya Nichrut ya kwao Zimbabwe.

Tshishimbi aumia mazoezini

Kiungo Mcongoman Papi Tshishimbi amepata majeraha katika mazoezi ya Yanga leo asubuhi uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro hivyo kumuweka kwenye hatihati ya kukosa mchezo wa kesho

Tshishimbi ameuamia enka, hatma ya kama kesho ataweza kucheza au la itategemea ripoti ya Daktari wa Yanga Dk Edward Bavu

Yanga itachuana na Mtibwa Sugar kesho Jumatano katika mchezo wa ligi kuu ambao utapigwa saa nane mchana kwenye uwanja wa Jamhuri

Makambo aipania Mtibwa Sugar

Heritier Makambo ameifungia Yanga mabao 15 kwenye ligi msimu huu akihitaji kufunga bao moja zaidi ili aweze kumfikia Salum Aiyee anayeongoza mbio za ufungaji bora akiwa amefunga mabao 16

Wakati ligi ikielekea ukingoni, mbio za kuwania kiatu cha dhahabu zimeendelea kupamba moto, Makambo akihitaji kutumia vyema michezo saba iliyobaki kufunga mabao mengi

Amefunga mabao matatu katika michezo miwili iliyopita na ameahidi kuendeleza moto wa mabao huko mkoani Morogoro Yanga itakapoikabili Mtibwa Sugar keshokutwa

Mcongomani huyo anawania nafasi ya kuitwa kikosi cha timu ya Taifa ya DR Congo kitakachoshiriki fainali za michuano ya AFCON 2019 zitakazofanyika mwezi Juni nchini Misri

Mwezi uliopita Makambo aliitwa kwenye kikosi cha awali cha DR Congo lakini hakufanikiwa kupenya kwenye orodha ya kikosi cha wachezaji 23 kilichoifunga Liberia 1-0 na kukata tiketi ya fainali hizo ambazo Tanzania pia itashiriki baada ya kusubiri kwa miaka 39

Simba kucheza mechi saba kwa wiki mbili ligi kuu

KeshoJumatano Simba inarejea rasmi kwenye mchakamchaka wa ligi kuu ya Tanzania Bara kwa kuikabili Coastal Union katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga

Kutokana na muda mchache uliobaki kabla ya ligi hiyo kumalizika mwezi ujao, Simba inakabiliwa na ratiba ya kucheza mfululizo ambapo katika kipindi cha wiki mbili itashuka dimbani mara saba

Baada ya mchezo dhidi ya Coastal Union April 17, mchezo utakaofuata ni dhidi ya Kagera Sugar utakaopigwa mkoani Kagera katika uwanja wa Kaitaba April 20

April 23 Simba itakuwa Mwanza kuchuana na Alliance Fc katika mchezo utakaopigwa uwanja wa CCM Kirumba kisha kurudi dimbani hapo April 26 kumenyana na KMC

Siku mbili baadae April 28 Simba itaelekea mkoani Mara kuikabili Biashara United kabla ya kuelekea mkoani Mbeya ambako May 01 itacheza na Tanzania Prisons kwenye uwanja wa Sokoine kisha kurejea tena dimbani hapo May 03 kuumana na Mbeya City