Category: michezo
Azam Fc vs Yanga kupigwa uwanja wa Uhuru

Mratibu wa Yanga Hafidh Saleh amesema wamepokea barua kutoka TFF inayowaelekeza sababu ya mchezo huo kuhamishiwa uwanja wa Uhuru ni kutoa nafasi kwa uwanja wa Taifa kufanyiwa ukarabati baada ya kumalizika mchezo wa fainali AFCON U17 utakaopigwa April 28 2019
Kikosi cha Yanga kinaendelea kujifua kwenye uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini jijini Dar es salaam kujiandaa na mchezo huo utakaopigwa Jumatatu, April 29 2019 saa kumi kamili jioni
Uwanja wa Uhuru ulifanyiwa ukarabati kabla ya kuanza kwa michuano ya vijana ya AFCON ambapo nyasi bandia za uwanja huo zilibadilishwa
Waliochangia Milioni moja kualikwa tukio kubwa May 11 Dar

Kutokana na umuhimu wa Kila Mwanayanga ambae anatoa pesa yake kwa ajili ya timu yetu TUIPENDAYO na yenye Thamani kubwa sana kwetu sote, Kamati imefikia uamuzi ufuatao ili kujenga wigo mpana wa kila mtu kuwa sehemu ya tukio hili muhimu linalohusu uchangiaji wa Klabu yetu.
Tukio Maalum la chakula cha jioni jijini Dar es salaam litafanyika siku ya Jumamosi tarehe 11/05/2019 Hotel ya Serena kuanzia saa kumi na mbili jioni.
Makundi ambayo yatakuwa yameshachangia shilingi milioni moja au zaidi yatapewa kadi ya mualiko na kumteua mtu mmoja ambaye ataliwakilisha kwa niaba na hatimaye aweze kushiriki kwenye Chakula Cha Jioni pamoja na kupokea CHETI MAALUMU cha Shukurani kwa niaba ya kundi lake.
Kamati imeona ni busara kupata uwakilishi huo wa mtu mmoja mmoja kutokana na eneo husika kubeba idadi isiyozidi watu mia tano.
Kwa mantiki hiyo tunaamini tutakuwa tumeweza kushirikisha kila kundi au mtu kwenye matukio haya muhimu kwa Klabu yetu.
TUENDELEE KUICHANGIA TIMU YETU ILI TUWE NA KIKOSI SHINDANI MSIMU UJAO
Timu ya Wananchi Wawekezaji ni Wananchi
Deo Mutta
KATIBU – KAMATI YA HAMASA
YANGA 23/04/2019
Yanga yajitathmini faini za kila mara

Matukio ya kutotumia mlango rasmi wa kuingia uwanjani yameigharimu sana Yanga msimu huu ambapo jana ilipigwa faini ya nne baada ya kufanya kosa hilo mkoani Mtwara ilipokwenda kucheza na Ndanda Fc
Yanga tayari imepigwa faini zilizoigharimu timu hiyo zaidi ya Tsh Milioni 10 kutokana na matukio hayo ya kuingia uwanjani kwa kutumia ‘njia za panya’
Afisa Habari wa Yanga Dismas Ten amesema matukio hayo yanachangiwa zaidi ya Wananchi ambao kimsingi ndio wenye timu na wanahusishwa kuisimamia timu inapokwenda kucheza
“Umefika wakati sasa tunapaswa kuwaelimisha watu wetu wafahamu athari tunazopata kutokana na kuendekeza imani hizi,” amesema
“Lazima ifahamike kila mchezo una kanuni na taratibu zake. Tukiendelea kuvunja kanuni kutokana na imani zetu, tutaendelea kuigharimu timu”
Simba dimbani leo kuikabili KMC

Baada ya juzi kuichapa Alliance Fc mabao 2-0 kwenye uwanja huo, leo Simba inarejea tena ikiwa na shauku ya kuondoka na alama zote tatu
Kocha Mkuu wa mabingwa hao watetezi Patrick Aussems amesema wanatarajia kupata upinzani mkali kutoka kwa KMC lakini wamejipanga kupata matokeo yatakayowapandisha hadi nafasi ya pili katika msimamo wa ligi
Ushindi utaiwezesha Simba kufikisha alama 66 na kuiondoa Azam Fc katika nafasi ya pili kutokana na wingi wa mabao ya kufunga
Katika mchezo wa duru ya kwanza uliopigwa uwanja wa Taifa, Simba ilifanikiwa kuondoka na alama zote tatu kwa ushindi wa mabao 2-1 huku ikifanya mabadiliko makubwa ya kikosi chake
Leo pia Aussems amesema atafanya mabadiliko ya kikosi kwani mchezo wa leo unahitaji uzoefu na ufundi
TMA yatoa tahadhari ujio wa kimbunga Keneth

Kwa mujibu wa TMA, jana kimbunga hicho kilikuwa kilomita 450 kutoka pwani ya Mtwara na kina kasi ya kilomita 130 kwa saa.
Kimbunga hicho kinatarajiwa kuongeza nguvu zaidi leo Alhamisi mchana ambapo kitakuwa kinasafiri kwa kilomita 170 kwa saa na kitakuwa kilomita 150 kutoka pwani ya Mtwara.
Kwa mujibu wa TMA, eneo husika ambalo kimbunga hicho kitatua litakuwa nchini Msumbiji, kikiwa na kasi ya kilomita 100 kwa saa. Eneo hilo litakuwa kilomita 200 kutoka pwani ya Mtwara.
Hata hivyo, mkoa wa Mtwara na maeneo jirani hususani mikoa ya Lindi na Ruvuma yataathirika pakubwa (athari zinategemewa kufikia umbali mpaka wa kilomita 500 kutoka Mtwara).
TMA imetahadharisha kuwa kimbunga hicho kitaingia nchi kavu na nguvu kubwa (ya upepo na mvua) itakayopelekea madhara makubwa kwa maisha ya watu na mali zao.
“Madhara yanayotarajiwa ni pamoja na mtawanyiko mkubwa wa mafuriko, uharibufu wa mali na makazi, kuezuliwa mapaa kutokana na upepo mkali. Uharibifu wa mazao mashambani na miundombinu kutokana na mafuriko”
Magazeti ya leo, Alhamisi, April 25 2019














Azam Fc vs Yanga mchezo usiotabirika

Huo utakuwa mchezo wa 19 kwa timu hizo kukutana kwenye ligi katika kipindi cha miaka 10
Katika michezo 18 iliyopita, Yanga na Azam Fc zimekuwa na matokeo sawa ambapo Yanga imeshinda michezo sita, Azam Fc ikishinda sita pia huku zikitoka sare mara sita
Hizi hapa takwimu za matokeo ya michezo iliyopita;
2008/09
Azam 1-3 Yanga (Oktoba 15, 2008)
Yanga 2-3 Azam (Aprili 8, 2009)
2009/10
Azam 1-1 Yanga (Oktoba 17, 2009)
Yanga 2-1 Azam (Machi 7,2010)
2010/11
Azam 0-0 (Okt 24, 2010)
Yanga 2-1 Azam (Machi 30, 2011)
2011/12
Azam 1-0 Yanga (Sept 18, 2011)
Yanga 1-3 Azam (Machi 10, 2012)
2012/13
Azam 0-2 Yanga (Nov 4, 2012)
Yanga 1-0 Azam (Feb 23, 2013)
2013/14
Azam 3-2 Yanga (Sept 22, 2013)
Yanga 1-1 Azam (Machi 19, 2014)
2014/15
Yanga 2-2 Azam (Des 28, 2014)
Azam 2-1 Yanga (Mei 5, 2015)
2015/16
Yanga 1-1 Azam (Okt 17,2015)
Azam 2-2 Yanga (Machi 5, 2016)
2017/2018
Azam fc 1-2 Yanga sc (Junuari 27/1/2017
Yanga 1-3 Azam Fc (May 28/5/2018
Katika kipindi cha misimu mitatu iliyopita, upinzani wa Yanga na Azam Fc umekuwa ukiongezeka hasa baada ya Azam Fc kuanza utamaduni wa kusajili wachezaji kutoka Yanga
Baada ya Azam Fc kuwasajili Didier Kavumbagu na Frank Domayo, mwaka juzi Yanga ilimnyakua Gadiel Michael
Mwaka jana Azam Fc iliwasajili Donald Ngoma aliyeachwa na Yanga na baadae Obrey Chirwa
Ngoma na Chirwa wanatarajiwa kuongoza safu ya ushambuliaji ya Azam Fc kwa mara ya kwanza kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Yanga
Chirwa aliifunga Yanga mapema mwaka huu kwenye michuano ya kombe la Mapinduzi katika mchezo ambao Azam Fc ilishinda mabao 3-0
Hata hivyo Yanga haikupeleka kikosi chake cha kwanza katika michuano hiyo ambayo Azam Fc iliibuka mabingwa
Ni mchezo ambao Yanga inahitaji kupata ushindi ili kuweka hai matumaini ya kutwaa ubingwa huku pia ikiiombea Simba iendelee kupunguzwa kasi katika michezo yake ya viporo
Matokeo tofauti na ushindi kwa Yanga huenda yakafifisha nafasi ya kutwaa ubingwa kwa vinara hao wa ligi kuu msimu huu
Azam Fc haina cha kupoteza kwani tayari imeshajiondoa katika kinyan’ganyiro cha kuwania ubingwa ikiweka mkazo zaidi kwenye michuano ya kombe la FA (ASFC)
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema mchezo huo hautakuwa mwepesi kutokana na ubora wa kikosi cha Azam Fc hata hivyo ni matokeo ya ushindi pekee ambayo yanaweza kuwapa nafasi ya kuwa mabingwa
“Hii ni mechi ngumu kwetu, Azam Fc ni timu nzuri ambayo ina ushindani wa hali ya juu. Tunafanya maandalizi maalum ili tuweze kuwafunga,naamini tukishinda tutajiweka katika mazingira mazuri zaidi ya kuchukua ubingwa,” amesema
Yanga inaongoza ligi ikiwa na alama 74, ikiwa mbele ya Azam Fc inayoshika nafasi ya pili kwa tofauti ya alama nane
Simba yakamilisha maandalizi ya kuikabili KMC

Mchezo huo utapigwa kesho Alhamisi kwenye uwanja wa CCM Kirumba
Simba ilishuka katika uwanja huo huo jana kuikabili Alliance Fc katika mchezo ambao Simba ilishinda kwa mabao 2-0
Baada ya mazoezi hayo yaliyosimamiwa na kocha Patrick Aussems, wachezaji walipewa mapumziko kusubiri mchezo huo wa kesho
Ratiba ya mabingwa hao watetezi haitoi nafasi kwa wachezaji kupata mapumziko ya kutosha hivyo benchi la ufundi kulazimika kupunguza muda wa mazoezi ili kuwapumzisha wachezaji





Hii hapa ‘bandika-bandua’ ya michezo ya Simba

Baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Alliance Fc jana, kesho Simba itashuka tena uwanja wa CCM Kirumba kuikabili KMC katika mchezo mwingine wa ligi kuu ya Tanzania Bara
Kocha Mkuu wa mabingwa hao watetezi Patrick Aussems amesema ataendelea kufanya ‘rotation’ ya kikosi chake ili kuhakikisha wanafikia malengo ya kutetea ubingwa
Hii hapa ratiba ya Simba kwa michezo iliyobaki mpaka mwishoni mwa msimu;
25/04/19 KMC Vs Simba SC .
27/04/19 Biashara Utd FC Vs Simba Sc.
30/04/19 Simba Sc Vs JKT Tanzania .
03/05/19 Mbeya City FC Vs Simba Sc.
06/05/19 Tanzania Prisons FC Vs Simba SC.
08/05/19 Simba SC Vs Coastal Union.
10/05/19 Simba SC Vs Kagera sugar FC.
13/05/19 Simba SC Vs Azam FC.
16/05/19 Simba SC Vs Mtibwa Sugar FC.
19/05/19 Simba SC Vs Ndanda FC.
22/05/19 Singida United vs Simba Sc.
25/05/19 Simba SC Vs Biashara United.
28/05/19 Mtibwa Sugar FC Vs Simba SC.










