Simba yajifua Mara

Kikosi cha Simba leo jioni kimefanya mazoezi kwenye uwanja wa Karume wilayani Musoma kujiandaa na mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Biashara United

Mchezo huo utapigwa kesho Jumamosi katika uwanja huo

Msafara wa Simba uliwasili mkoani Mara mapema leo na kupokewa na idadi kubwa ya mashabiki waliokuwa na shauku ya kuwaona mabingwa hao wa nchi

Simba yapata mapokezi makubwa Mara

Kikosi cha Simba kimewasili salama mkoani Mara tayari kwa mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Biashara United

Mchezo huo utapigwa kesho Jumamosi, April 27 kwenye uwanja wa Karume

Idadi kubwa ya mashabiki wamejitokeza kwa wingi kuulaki msafara wa mabingwa hao watetezi wakati ukiingia Musoma

Waamuzi mchezo wa KMC vs Simba waondolewa

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewaondoa waamuzi waliochezesha mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara kati ya KMC dhidi ya Simba uliopigwa jana uwanja wa CCM Kirumba


Kulingana na taarifa iliyotolewa na TFF, Waamuzi hao wanatuhumiwa kuchezesha mchezo huo chini ya kiwango
Katika mchezo huo Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-1

Mchezo wa Biashara United vs Simba utapigwa hapa

Simba kesho Jumamosi itandelea na ratiba yake ya ‘bandika-bandua’ kwa kuikabili Biashara United katika mchezo utakaopigwa dimba la Karume wilayani Musoma

Simba tayari imeondoka Mwanza na leo jioni inatarajiwa kujifua kwenye uwanja huo

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Simba kucheza mkoani Mara baada ya kupita miaka 15

Biashara United inanolewa na beki wa zamani wa Simba Amri Said

Manara awapasha Yanga, ‘kalipeni mishahara ya wachezaji wenu’

Afisa Habari wa Simba Haji Manara amewataka mashabiki wa Yanga watumie muda wao kuinusuru timu yao na ‘ukata’ uliowakumba kuliko kupoteza muda mwingi kuifuatilia Simba ambayo inafanikiwa mambo yake

Baada ya mchezo dhidi ya KMC jana, mashabiki wa Yanga walionekana kuisemea KMC kuwa imeonewa na waamuzi huku wachezaji wa timu yao wakigoma kufanya mazoezi wakidai mishahara

Tangu jana wachezaji wa Yanga hawafanyi mazoezi wakishinikiza walipwe madai yao ya mishahara ya miezi mitatu huku wengine wakiwa hawajalipwa fedha za usajili mpaka leo

“Badala ya kuhangaika jinsi ya kuwalipa mishahara wachezaji wenu mnahangaika na timu Bingwa inayowafunga kila siku. Kama nyie wananchi wachangieni hao wachezaji walipwe mishahara,” ameandika Manara kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram

Majanga ya msimu uliopita yaikumba tena Yanga

Wakati kikosi cha Yanga kikitarajiwa kuchuana na Azam Fc Jumatatu, April 29 katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara, kocha Mwinyi Zahera huenda akalazimika kutumia wachezaji wa kikosi cha pili kufuatia mgomo unaofanywa na wachezaji wa kikosi cha kwanza

Leo Zahera aliamua kutumia wachezaji wa Yanga B kujiandaa na mchezo dhidi ya Azam FC baada ya wachezaji wa kikosi cha kwanza kugoma tena kufanya mazoezi licha ya kufika mapema uwanja wa chuo cha Polisi Kurasini

Mwishoni mwa msimu uliopita Yanga ilikumbana na changamoto kama hii ya wachezaji kugoma wakishinikiza walipwe hali iliyopelekea kumalizia michezo ya mikaoni ikiwa na kikosi cha wachezaji 14

Huenda hali hiyo ikajirudia tena kwa michezo sita iliyobaki kama viongozi wa muda wa Yanga hawatachukua hatua za haraka kutatua mgogoro uliopo

Wachezaji wafika mazoezini kuendelea na maandalizi ya kuikabili Azam Fc

Wachezaji wote leo wamefika mazoezini kuendelea na maandalizi ya mchezo dhidi ya Azam Fc utakaopigwa Jumatatu, April 29 kwenye uwanja wa Uhuru

Jana wachezaji hao waligoma kufanya mazoezi wakishinikiza waonane na uongozi wa Yanga ili kujua hatma ya madai yao ya mishahara na fedha za usajili

Wagoma tena

Licha ya kufika mapema mazoezini, wachezaji wa kikosi cha kwanza, waligoma kufanya mazoezi wakiwasubiri viongozi wafanye nao kikao

Kocha Zahera alilazimika kutumia Yanga B kuendelea na program ya mazoezi kujiandaa na mchezo dhidi ya Azam

Penati hazina mwenyewe, tuwavumilie wachezaji wanapokosa

Katika mchezo wa kwanza wa ligi ya mabingwa dhidi ya TP Mazembe, nahodha John Bocco alikosa mkwaju wa penati tukio ambalo lilimfanya ashushiwe lawama nyingi na mashabiki

Hata hivyo leo katika mchezo dhidi ya KMC, Bocco ameifungia Simba mkwaju muhimu wa penati ulioipandisha Simba hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1

Hata hivyo katika mchezo huo Meddie Kagere alikosa penati ya kwanza iliyotolewa na mwamuzi

Matukio haya yanadhihirisha kuwa hakuna sababu ya kuwalaumu wachezaji pale wanapokosa mikwaju ya penati kwani hakuna mchezaji mwenye uhakika wa kufunga penati kwa asilimia 100

Katika kikosi cha Simba Bocco ndiye mwenye rekodi nzuri ya kufunga mikwaju ya penati.

Kwenye ligi Bocco amefunga mikwaju yote mitano aliyopiga msimu huu

Kiporo Kimeliwa Simba Waichapa KMC bao 2-1

Hayawi hayawi sasa yamekua ni katika muendelezo wa simba kula viporo ndani ya uwanja wa ccm kirumba mwanza leo timu ya simba ikiibuka na ushindi mnono wa bao mbili kwa moja huku.

Bao la kwanza la Simba limepatikana kutoka kwa Emmanuel Okwi dakika ya 23 na kusawazisha na mchezaji mahiri kabisa kutoka KMC Hassan kabunda mnamo dakika ya 57 baaadae kabisa dakika za lala salama John Bocco ameipatia goli la ushindi kwa mkwaju wa pelnati dakika ya 82.

Ni moja ya mchezo ulio kua na mvutano mkubwa kutoka pande zote mbili huku AK 14 Meddie Kagere akikosa penalt

Kwa matokea haya sasa simba imemfikia azam fc kwa kuwa na point sawa