Sevilla yaahirisha mchezo dhidi ya Singida United

May 23 2019 Simba itacheza mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Sevilla inayoshiriki ligi kuu ya Hispania maarufu kama La Liga

Hata hivyo kulingana na ratiba ya ligi iliyotolea awali na Bodi ya Ligi, May 22 Simba ilipaswa kuwa mkoani Singida kucheza na Singida United

Bodi ya ligi imelazimika kuahirisha mchezo huo dhidi ya Singida United

Huenda Simba ikacheza na Singida United baada ya mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa May 28 kwani baada ya kuikabili Sevilla, May 25 Simba itacheza na Biashara United mchezo utakaopigwa uwanja wa Taifa

Simba yasaka alama tatu dhidi ya Mbeya City leo

Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba wako mkoani Mbeya ambapo leo watashuka dimba la Sokoine kuwakabili wenyeji wao Mbeya City

Simba inayoshika nafasi ya pili baada ya kujikusanyia alama 72, inahitaji ushindi katika michezo saba tu ili kuubakisha ubingwa Msimbazi

Msemaji wa Simba Haji Manara amesema wachezaji wa timu hiyo wako katika hali nzuri tayari kwa mchezo huo

“Timu imewasili salama mkoani Mbeya tayari kwa mchezo. Tunafahamu hautakuwa mchezo mwepesi lakini wachezaji wetu watapambana kuhakikisha tunaondoka na alama zote tatu,” amesema

Katika mchezo wa leo, Simba itamkosa nahodha wake John Bocco ambaye aliumia kwenye mchezo uliopita dhidi ya JKT Tanzania

Wengine watakaokosekana ni Asante Kwasi, Paschal Wawa na Shomari Kapombe

Baada ya mchezo huo Simba itaendelea kubaki mkoani Mbeya ambapo keshokutwa May 05 itachuana na Tanzania Prisons

Simba yamlilia Dk Mengi

Uongozi wa klabu ya Simba umepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dk Reginald Mengi kilichotokea jana Dubai

Taarifa iliyotolewa na Simba imesema klabu inaungana na familia na Watanzania katika kuomboleza msiba huo mkubwa

Simba yawasili salama Mbeya

Msafara wa kikosi cha Simba umewasili salama mkoani Mbeya tayari kwa michezo miwili ya ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Mbeya City na Tanzania Prisons

Simba iliondoka jijini Dar es salaam mchana wa leo Alhamisi kwa usafiri wa Ndege

Kesho May 03 itacheza mchezo wa kwanza dhidi ya Mbeya City kwenye uwanja wa Sokoine na siku mbili baadae kurudi tena katika uwanja huo kuikabili Tanzania Prisons

Prisons iko jijini Dar es salaam ambapo leo imecheza na Yanga na kufungwa mabao 2-1, itachuana na Simba May 05

Makambo awafikia Aiyee, Kagere

Bao alilofunga Heritier Makambo katika mchezo dhidi ya Tanzania Prisons limemfanya mshambuliaji huyo afikishe mabao 16 na kuwafikia Salum Aiyee wa Mwadui Fc na Meddie Kagere wa Simba

Leo Makambo ameiongoza Yanga kuibuka na ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Tanzania Prisons

Mshambuliaji huyo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, anayo nafasi ya kuibuka mfungaji bora msimu huu kama ataweza kuitumia vyema michezo minne iliyobaki kujiongezea mabao

Michezo iliyobaki ni dhidi ya Ruvu Shooting, Mbeya City, Biashara United na Azam Fc

Ni mchezo mmoja tu dhidi ya Biashara United ambao utapigwa nje ya jiji la Dar es salaam

Wawa aanza mazoezi, kurejea kikosini karibuni

Beki kisiki wa Simba Paschal Serge Wawa ameanza mazoezi mepesi tayari kurejea dimbani baada ya kuwa nje kwa zaidi ya wiki tatu

Wawa aliumia kwenye mchezo wa kwanza wa robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kati ya Simba dhidi ya TP Mazembe uliopigwa uwanja wa Taifa

Wawa ameanza mazoezi binafsi na huenda akajumuishwa kwenye kikosi cha Simba kitakaporudi kutoka mkoani Mbeya

Mwenyewe amethibitisha kuwa hali yake inaendelea vizuri na tayari ameshaanza mazoezi binafsi

“Ninaendelea vizuri kwa sasa tofauti na awali na nimeanza mazoezi binafsi na sasa hivi ninafanya mazoezi ya Gmy,” amesema

Simba imecheza michezo sita ya ligi bila ya Wawa na imefanikiwa kushinda michezo mitano

Walinzi Juuko Murshidi, Paul Bukaba na Yusufu Mlipili wameweza kutimiza ipasavyo majukumu ya ulinzi wa kati wakishirikiana na mkongwe kiraka Erasto Nyoni

Sevilla itawajengea wachezaji uzoefu wa Kimataifa

Mafanikio ya Simba kwenye michuano ya SportPesa Super Cup msimu huu yameipelekea mabingwa hao wa Tanzania Bara kuteuliwa kuivaa Sevilla katika mchezo wa Kimataifa wa kirafiki utakaopigwa May 23 jijini Dar es salaam

Uongozi wa Simba umesema mchezo huo ni fursa adimu kwa wachezaji wake kwani utawasaidia kuwajengea uzoefu wa Kimataifa

Aidha Simba imesema itautumia mchezo huo kuitangaza Tanzania Kimataifa kwani wanajua utafuatiliwa na mamilioni ya mashabiki wa soka duniani kwani utarushwa mbashara na runinga mbalimbali kote duniani

Msemaji wa klabu ya Simba Haji Manara amesema uteuzi huo ni sahihi kwa Simba kwani ukiachilia mbali mafanikio waliyopata kwenye michuano ya SportPesa ukilinganisha na timu nyingine za Tanzania, Simba iko kwenye kiwango cha juu zaidi kwa sasa hapa nchini

“Simba kwa sasa ipo katika kiwango cha juu na kucheza na Sevilla kutasaidia kujua viwango vya wachezaji wetu katika mechi za kimataifa,” amesema

“Mechi hii inaiweka Tanzania katika historia kubwa sana katika soka. Historia zinaonyesha kuwa miaka ya nyuma, timu mbalimbali kutoka nje ya mipaka ya Afrika zilikuja hapa Tanzania na kucheza na Yanga na Simba, miaka ya hivi karibuni hakukuwa na ujio huo zaidi ya mwaka 2017 ambapo SportPesa iliileta timu ya Everton na kucheza timu ya Gor Mahia ya Kenya”

Sevilla ni moja ya timu kongwe na maarufu nchini Hispania na barani Ulaya. Imewahi kutwaa taji la Europa kwa misimu mitatu mfululizo katika kipindi cha miaka mitano iliyopita

Simba yaelekea mkoani Mbeya

Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Tanzania Bara, Simba wanaondoka asubuhi hii kuelekea mkoani Mbeya tayari nkwa michezo miwili ya ligi dhidi ya Mbeya City na Tanzania Prisons

Kesho Ijumaa May 03, Simba itashuka uwanja wa Sokoine kuikabili Mbeya City kisha kurejea tena katika uwanja huo May 05 kuikabili Tanzania Prisons

Ikiwa imesalia na michezo 10, Simba inahitaji kushinda michezo saba tu ili iweze kutetea ubingwa wake kwa msimu wa pili mfululizo

Hii hapa ratiba ya michezo yote iliyobaki