Simba na yanga zajitoa mashindano ya cecafa ,yatakayofanyika Rwanda mwaka huu

credit: @sokawaytz…

✍🏻 Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye amesisitiza kuwa mashindano ya Kombe la Kagame yatafanyika kama ilivyopangwa licha ya vilabu kujitoa kwa Sababu Mbalimbali; Mabingwa wa Tanzania, Simba SC, walikuwa wa kwanza kutangaza kujitoa katika Mashindano hayo wiki iliyopita, na leo Jumapili wapinzani wao, Yanga SC pia wamethibitisha kuwa hawatoshiriki katika mashindano hayo ya kikanda.. Jana Mabingwa wa Burundi, Agle Noir FC waliandika barua ya kujitoa.

.

– Mechi za Mashindano haya zinatarajiwa kufanyika jijini Kigali, Rwanda kuanzia Julai 7 mpaka Julai 21..

🗣 (Simba na Yanga) “Haishangazi hata wanapopigwa katika mashindano ya CAF, mara zote hupoteza kwa 5-0 au hata 6-0, hatufadhaiki wala haitukwamishi kwa kujitoa kwao”… Alisema Musonye ambapo Pia amesisitiza kuwa tayari wana timu kadhaa kutoka Kenya, Uganda, Rwanda na DR Congo ambazo zitakuja na kujaza nafasi hizo timu mbili za Tanzania.

🗣 “Mashindano hayawezi kushindwa kufanyika kwa sababu ya Yanga na Simba hawapo, na tayari tumezungumza na timu Mbalimbali kuja kushiriki badala yao, Lengo letu ni kuwa na mashindano ya timu 16 na tutasimamia yawe hivyo” Musonye amesema.

.

✍🏻 Zesco United ya Zambia, AS Vita Club na DC Motema Pembe za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wao tayari wamethibitisha ushiriki wao pamoja na Azam FC ya Tanzania… Mashindano huleta timu kutoka Kenya, Rwanda, Burundi, Djibouti, Eritrea, Sudan, Somalia, Sudan Kusini, Ethiopia, Uganda, Tanzania na Zanzibar… Mshindi wa mashindano haya atarejea nyumbani kwake na kitita cha pesa ya thamani ya US$30,000..

#Updates #kagameCup

@Sokawaytz

Meddie kagere akabidhiwa kiatu chalet cha ufungaji bora

credit: @simbasctanzania…

Meddie Kagere amekabidhiwa Tuzo ya Mfungaji Bora na tovuti ya habari za michezo ya Kandanda. Katika msimu wa Ligi Kuu 2018/2019 ambao umemalizika hivi karibuni, Kagere alimaliza akiwa amefunga magoli 23 ambayo yamemwezesha kuwa mfungaji bora. #NguvuMoja

Simba yampa mtihani Meddie Kagere avunje rekodi ya Abdallah Juma kwa ufungaji msimbazi

“Amekuwa na msimu mzuri na anapambana muda wote, nadhani ataweza kufunga mabao mawili katika mchezo uliobaki na kuifikia rekodi ya Abdallah Juma nasi wachezaji tutamsaidia kwakua tunashirikiana sana,” Nahodha wa Simba, John Bocco akimzungumzia Meddie Kagere kuelekea kufikia rekodi ya ufungaji ya Abdallah Juma kwenye ligi kuu. Kwa sasa Kagere ana mabao 23.

credit: @simbamakini

Okwi awashitua mashabaki wa simba sc clubs

✋ Emmanuel Okwi juu ya Ujumbe wake katika mtandao wa Instagram uliozua sintofahamu kwa Mashabiki wake na Klabu yake ya @simbasctanzania kwamba je ni kweli ameaga kuachana Mabingwa hao.

:

👉 “Nimeweka ujumbe huo sikuwa na maana yoyote zaidi ya wimbo mmoja ambao naupenda na umejizolea umaarufu na wapenzi wa Simba wasiwe na wasiwasi wowote kuhusu hilo,” alisema Okwi.

.

– Okwi amekuwa akihusishwa kutimka ndani ya Klabu ya @simbasctanzania Kipindi hiki ambacho Mazungumzo ya Kusaini Mkataba mpya na Klabu yake yamepungua.. @kcfcofficial ya Afrika Kusini ndio Klabu inayotajwa kumuhitaji.

#simbasc #transfers

@Sokawaytz

credit: @sokawaytz