ADAM SALAMBA: Kuweka Kumbukumbu kiatu cha Banega

Baada ya mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Sevilla, tukio la mshambuliaji wa Simba Adam Salamba kumuomba kiatu kiungo mahiri na nahodha wa Sevilla Ever Banega, liliibua mijadala kwenye mitandao ya kijamii

Baadhi ya mashabiki hawakuelewa maana ya tukio hilo ambalo ni la kawaida na hufanywa na wanasoka kama sehemu ya kuonyesha uungwana mchezoni

Salamba amesema ataweka kumbukumbu kiatu alichopewa na kiungo huyo wa Kimataifa wa Argentina

“Kiatu ambacho nimepewa na mchezaji wa kimataifa kutoka Sevilla, Ever Banega nitakichongea fremu iwe kumbukumbu daima,” amesema

Aidha Salamba amesema fursa ya kucheza na Sevilla imemuongezea shauku ya kutaka kwenda kucheza soka nje ya nchi

“Ndoto zangu ni kucheza nje ya Tanzania, baada ya kucheza na Sevilla juzi, imeniongezea ari ya kutaka kufikia malengo hayo”

Francis Kahata amegoma kuongeza mkataba katika klabu hiyo huku akihusishwa kusajiliwa na Simba mkataba wake utakapomalizika mwezi wa saba

Kiungo fundi wa Gor Mahia Francis Kahata amegoma kuongeza mkataba katika klabu hiyo huku akihusishwa kusajiliwa na Simba mkataba wake utakapomalizika mwezi wa saba

Msimu huu Kahata ameisaidia Gor Mahia kutwaa taji la ligi kuu ya Kenya pamoja na kuisaidia timu hiyo kufika hatua ya robo fainali kombe la Shirikisho Barani Afrika

Hata hivyo fundi huyo wa mpira anataka kuungana na Meddie Kagere mshambuliaji wa zamani wa Gor Mahia ambaye kwa sasa yuko Simba

Inaelezwa Kagere amemshawishi kiungo huyo ambaye walicheza nae katika klabu ya Gor Mahia

Gor Mahia inakabiliwa na hali ngumu ya kiuchumi na huenda ikawapoteza nyota wake muhimu wanaowania na timu kadhaa

Mshambuliaji tegemeo wa timu hiyo Jacques Tuyisenge yuko mbioni kukamilisha usajili kunako klabu ya Atletico De Luanda ya nchini Msumbiji

Baada ya kumkosa msimu uliopita, Simba ina nafasi nzuri ya kumsajili Kahata msimu huu

BOCCO Ataka Shangwe za Ubingwa zihamie Morogoro

Jana mashabiki wa Simba waliojitokeza uwanja wa Taifa kushuhudia ‘mnyama’ akikabidhiwa kombe baada ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu, hawakufurahia kuahirishwa kwa hafla hiyo

Licha ya mvua kunyesha, baadhi ya mashabiki walikubali ‘kulowana’ ili mradi tu washuhudie tukio hilo la kihistoria

Hata hivyo Bodi ya ligi iliahirisha hafla hiyo baada ya mgeni rasmi, Waziri wa Mambo ya Ndani Mh Kangi Lugola kupata udhuru

Mtendaji wa Bodi ya Ligi Boniface Wambura alisema sherehe hizo zimehamishiwa mkoani Morogoro, zitafanyika baada ya mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa keshokutwa Jumanne katika uwanja wa Jamhuri

Akingumza baada ya mchezo dhidi ya Biashara United uliomalizika kwa sare ya bao 1-1, nahodha wa Simba John Bocco aliwashukuru mashabiki waliojitokeza uwanja wa Taifa kuwaunga mkono licha ya hali ya mvua

FT: Simba 1-1 Biashara United

Mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara kati ya Simba, mabingwa msimu huu na Biashara United umemalizika kwa timu hizo kutoka sare ya kufungana bao 1-1

Mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa Taifa, ulivurugwa na mvua zilizojaza maji katika sehemu ya kuchezea ya dimba la Mkapa

Biashara United ilitangulia kupata bao la kuongoza kupitia kwa Innocent Edwin kwenye dakika ya 14 na Simba ikasawazisha dakika tatu baadae kupitia kwa Clatous Chama

Mashabiki hawakujitokeza kwa wingi uwanjani kutokana na hali ya mvua inayoendelea kunyesha jijini Dar es salaam

Yatibua sherehe za ubingwa

Bodi ya Ligi imelazimika kuahirisha sherehe za kuwakabidhi Simba kombe kutokana na changamoto ya mvua

Aidha Mtendaji wa Bodi Boniface Wambura amesema mgeni Rasmi Mh Kangi Lugola naye alipata dharura

Simba sasa itakabidhiwa ubingwa mkoani Morogoro siku ya Jumanne, itakapochuana na Mtibwa Sugar katika mchezo wa kumaliza msimu

Uongozi wa Simba umewataka mashabiki wa timu hiyo mkoani Morogoro kujiandaa kuipokea timu na kuwa tayari kwa shamrashamra za kihistoria

Sherehe za Ubingwa Simba Kufanyika Leo

Mabingwa wa nchi Simba leo wanakabidhiwa taji la pili mfululizo ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya mchezo dhidi ya Biashara United

Mchezo huo utaanza mapema tu, saa tisa Alasiri ambapo hafla ya makabidhiano ya ubingwa itafanyika baada ya mchezo huo

Waziri wa Mambo ya Ndani Mh Kangi Lugola anatarajiwa kuwa mgeni wa rasmi katika hafla hiyo itakayofanyika uwanja wa Taifa

Uongozi wa Simba umewataka mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanja wa Taifa leo kushuhudia tukio hilo litakalobaki kwenye kumbukumbu za klabu ya Simba

Hilo ni taji la 20 la ligi kuu ya Tanzania Bara kwa Simba

Baada ya kuichachafya Sevilla juzi, Aussems amepania kushusha mziki kamili ili kunogesha sherehe za ubingwa kwa ushindi mnono

Viingilio vya mchezo huo, VIP A Tsh 15,000/- VIP B na C Tsh 10,000/- wakati mzunguuko ni Tsh 3,000/-

Kocha wa Sevilla Amvulia Kofia John Bocco, Adai Ana Kiwango Kama cha Drogba

Mkufunzi wa sevia kutoka laliga ya Spain ameshangazwa na uwezo wa john boco drogba kwa kysema hakudhania Kama Tanzania kuna vipaja namna hii!!

Alisema namnukuu “I have never been in east Africa especially Tanzania, I used to know some talented from Africa like drogba and keita but to me that young man with number 22 kit is really magnetic, classical and professional”

Reporter: would you ever sign him?

Why not’ any manager would like to work with “booock’o (Spanish articulation) but i know it is not easy to sign a player from simba which is the richest club in central and east africa

Reporter, three players from simba with best performance tonight boco excluded?

I think kaaagere, nyoni and mkuude performed well

Huyu boco hatari sana tusishangae kesho akalambishwa mkataba na sevia’

Kila la kheri boko umri unaruhusu Wewe bado kijana mdogo na haujapunguza umri