Klabu ya Simba Sc imeanza kuwania saini ya beki wa Lipuli Fc Willium Lucian “Galas” ili kuboresha kikosi chao kuelekea kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika msimu ujao. .
Taarifa za awali zinadai kuwa huenda ikaachana na beki wao Zana Coulibaly.
Category: simba
Lamine Moro beki raia wa Ghana ambaye awali aliwahi kufanya majaribio na kikosi cha Simba Sc ametua nchini kumalizana na Yanga Sc tayari kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania.
Lamine Moro beki raia wa Ghana ambaye awali aliwahi kufanya majaribio na kikosi cha Simba Sc ametua nchini kumalizana na Yanga Sc tayari kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania.
ADAM SALAMBA: Kuweka Kumbukumbu kiatu cha Banega
Baada ya mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Sevilla, tukio la mshambuliaji wa Simba Adam Salamba kumuomba kiatu kiungo mahiri na nahodha wa Sevilla Ever Banega, liliibua mijadala kwenye mitandao ya kijamii
Baadhi ya mashabiki hawakuelewa maana ya tukio hilo ambalo ni la kawaida na hufanywa na wanasoka kama sehemu ya kuonyesha uungwana mchezoni

Salamba amesema ataweka kumbukumbu kiatu alichopewa na kiungo huyo wa Kimataifa wa Argentina
“Kiatu ambacho nimepewa na mchezaji wa kimataifa kutoka Sevilla, Ever Banega nitakichongea fremu iwe kumbukumbu daima,” amesema
Aidha Salamba amesema fursa ya kucheza na Sevilla imemuongezea shauku ya kutaka kwenda kucheza soka nje ya nchi
“Ndoto zangu ni kucheza nje ya Tanzania, baada ya kucheza na Sevilla juzi, imeniongezea ari ya kutaka kufikia malengo hayo”
Francis Kahata amegoma kuongeza mkataba katika klabu hiyo huku akihusishwa kusajiliwa na Simba mkataba wake utakapomalizika mwezi wa saba
Kiungo fundi wa Gor Mahia Francis Kahata amegoma kuongeza mkataba katika klabu hiyo huku akihusishwa kusajiliwa na Simba mkataba wake utakapomalizika mwezi wa saba
Msimu huu Kahata ameisaidia Gor Mahia kutwaa taji la ligi kuu ya Kenya pamoja na kuisaidia timu hiyo kufika hatua ya robo fainali kombe la Shirikisho Barani Afrika
Hata hivyo fundi huyo wa mpira anataka kuungana na Meddie Kagere mshambuliaji wa zamani wa Gor Mahia ambaye kwa sasa yuko Simba
Inaelezwa Kagere amemshawishi kiungo huyo ambaye walicheza nae katika klabu ya Gor Mahia
Gor Mahia inakabiliwa na hali ngumu ya kiuchumi na huenda ikawapoteza nyota wake muhimu wanaowania na timu kadhaa
Mshambuliaji tegemeo wa timu hiyo Jacques Tuyisenge yuko mbioni kukamilisha usajili kunako klabu ya Atletico De Luanda ya nchini Msumbiji
Baada ya kumkosa msimu uliopita, Simba ina nafasi nzuri ya kumsajili Kahata msimu huu
BOCCO Ataka Shangwe za Ubingwa zihamie Morogoro
Jana mashabiki wa Simba waliojitokeza uwanja wa Taifa kushuhudia ‘mnyama’ akikabidhiwa kombe baada ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu, hawakufurahia kuahirishwa kwa hafla hiyo
Licha ya mvua kunyesha, baadhi ya mashabiki walikubali ‘kulowana’ ili mradi tu washuhudie tukio hilo la kihistoria
Hata hivyo Bodi ya ligi iliahirisha hafla hiyo baada ya mgeni rasmi, Waziri wa Mambo ya Ndani Mh Kangi Lugola kupata udhuru
Mtendaji wa Bodi ya Ligi Boniface Wambura alisema sherehe hizo zimehamishiwa mkoani Morogoro, zitafanyika baada ya mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa keshokutwa Jumanne katika uwanja wa Jamhuri
Akingumza baada ya mchezo dhidi ya Biashara United uliomalizika kwa sare ya bao 1-1, nahodha wa Simba John Bocco aliwashukuru mashabiki waliojitokeza uwanja wa Taifa kuwaunga mkono licha ya hali ya mvua
FT: Simba 1-1 Biashara United
Mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara kati ya Simba, mabingwa msimu huu na Biashara United umemalizika kwa timu hizo kutoka sare ya kufungana bao 1-1
Mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa Taifa, ulivurugwa na mvua zilizojaza maji katika sehemu ya kuchezea ya dimba la Mkapa
Biashara United ilitangulia kupata bao la kuongoza kupitia kwa Innocent Edwin kwenye dakika ya 14 na Simba ikasawazisha dakika tatu baadae kupitia kwa Clatous Chama

Mashabiki hawakujitokeza kwa wingi uwanjani kutokana na hali ya mvua inayoendelea kunyesha jijini Dar es salaam
Yatibua sherehe za ubingwa
Bodi ya Ligi imelazimika kuahirisha sherehe za kuwakabidhi Simba kombe kutokana na changamoto ya mvua
Aidha Mtendaji wa Bodi Boniface Wambura amesema mgeni Rasmi Mh Kangi Lugola naye alipata dharura
Simba sasa itakabidhiwa ubingwa mkoani Morogoro siku ya Jumanne, itakapochuana na Mtibwa Sugar katika mchezo wa kumaliza msimu
Uongozi wa Simba umewataka mashabiki wa timu hiyo mkoani Morogoro kujiandaa kuipokea timu na kuwa tayari kwa shamrashamra za kihistoria
HIKI HAPA KIKOSI CHA SIMBA KITAKACHO CHEZA LEO DHIDI YA BIASHARA UNITED



Sherehe za Ubingwa Simba Kufanyika Leo
Mabingwa wa nchi Simba leo wanakabidhiwa taji la pili mfululizo ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya mchezo dhidi ya Biashara United
Mchezo huo utaanza mapema tu, saa tisa Alasiri ambapo hafla ya makabidhiano ya ubingwa itafanyika baada ya mchezo huo
Waziri wa Mambo ya Ndani Mh Kangi Lugola anatarajiwa kuwa mgeni wa rasmi katika hafla hiyo itakayofanyika uwanja wa Taifa
Uongozi wa Simba umewataka mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanja wa Taifa leo kushuhudia tukio hilo litakalobaki kwenye kumbukumbu za klabu ya Simba
Hilo ni taji la 20 la ligi kuu ya Tanzania Bara kwa Simba
Baada ya kuichachafya Sevilla juzi, Aussems amepania kushusha mziki kamili ili kunogesha sherehe za ubingwa kwa ushindi mnono
Viingilio vya mchezo huo, VIP A Tsh 15,000/- VIP B na C Tsh 10,000/- wakati mzunguuko ni Tsh 3,000/-
Kocha wa Sevilla Amvulia Kofia John Bocco, Adai Ana Kiwango Kama cha Drogba
Mkufunzi wa sevia kutoka laliga ya Spain ameshangazwa na uwezo wa john boco drogba kwa kysema hakudhania Kama Tanzania kuna vipaja namna hii!!
Alisema namnukuu “I have never been in east Africa especially Tanzania, I used to know some talented from Africa like drogba and keita but to me that young man with number 22 kit is really magnetic, classical and professional”
Reporter: would you ever sign him?
Why not’ any manager would like to work with “booock’o (Spanish articulation) but i know it is not easy to sign a player from simba which is the richest club in central and east africa
Reporter, three players from simba with best performance tonight boco excluded?
I think kaaagere, nyoni and mkuude performed well
Huyu boco hatari sana tusishangae kesho akalambishwa mkataba na sevia’
Kila la kheri boko umri unaruhusu Wewe bado kijana mdogo na haujapunguza umri
LUGOLA – Mgeni Rasmi Sherehe za UBINGWA – SIMBA
Simba kesho itakabidhiwa ubingwa wa ligi kuu baada ya mchezo dhidi ya Biashara United utakaopigwa uwanja wa Taifa kuanzia saa tisa Alasiri
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza mgeni wa heshima wa mchezo huo atakuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Mh Kangi Lugola










