
































Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Jumapili, March 31 na huenda ukapigwa kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro
Mazoezi ya leo yalihusisha wachezaji ambao hawakuitwa katika timu za Taifa



Baada ya kufuzu jana, Tanzania itakuwa miongoni mwa timu 24 zitakazopangwa katika makundi sita ya timu nne nne kuwania ubingwa wa Afrika
Timu zote zilizofuzu;


Jana Zahera akiwa kocha msaidizi wa timu ya Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, alikiongoza kikosi cha timu hiyo kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Liberia na kukata tiketi ya kufuzu fainali za AFCON 2019
Mwishoni mwa wiki hii Yanga itaelekea mkoani Mwanza kuikabili Alliance Fc katika mchezo utakaopigwa dimba la CCM Kirumba, March 30 2019
Kwa sasa Yanga inajifua chini ya kocha msaidizi Noel Mwandila
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa serikali itatoa shilingi bilioni moja kwaajili ya kuiwezesha Serengeti Boys.
Rais Magufuli amesema kuwa atatoa fedha hizo ili kuiwezesha timu hiyo kufanya vizuri kwenye mashindano ya Afrika kwa vijana AfconU17 yatakayofanyika nchini Tanzania mwezi Aprili mwaka huu.
Rais Magufuli amesema kuwa ataendelea kushirikiana na Wizara ya Michezo kwa kuwa Timu ya Taifa Stars imemfurahisha sana baada ya kuipiga timu ya Uganda 3 bila.

Kulingana na taarifa iliyotolewa mapema leo na msemaji wa Ikulu Gerson Msigwa, Rais Magufuli atatoa pongezi kwao na kula nao chakula cha mchana
Jana Stars ilifanikiwa kufuzu fainali za AFCON 2019 baada ya kusubiri kwa miaka 39 ikiibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Uganda katika mchezo uliopigwa uwanja wa Taifa


Stars imefuzu kwa fainali hizo baada ya kusubiri kwa miaka 39
Matokeo ya suluhu ya bila kufungana kati ya Cape Verde dhidi ya Lesotho yameinufaisha Tanzania kuweza kuwa miongoni mwa timu 24 zitakazochuana nchini Misri mwezi Juni
Stars iliyokuwa katika kiwango bora, iliandika bao la kuongoza kwenye dakika ya 21 kupitia kwa Saimon Msuva aliyemalizia pasi murua ya John Bocco
Erasto Nyoni akaifungia Stars bao la pili kupitia mkwaju wa penati kwenye dakika ya 50 baada ya Samatta kumnawisha mlinzi wa Uganda ndani ya eneo la hatari
Bao lililoizamisha Uganda liliwekwa kimiani na Aggrey Morisi kwenye dakika ya 56 akimalizia krosi iliyochongwa na John Bocco
Ushindi wa Stars ulinogeshwa na idadi kubwa ya mashabiki waliofurika kuujaza uwanja wa Taifa
Kikosi cha Stars kilichoandika historia leo;
Manula, Hassan Kessy, Gadiel Michael, Agrey Morris, Kelvin Yondani, Erasto Nyoni , Saimon Msuva, Mudathir Yahya, John Bocco, Mbwana Samatta, Farid Mussa
AKIBA
Metacha Munata, Aron Kalambo, Ally Sonso, Kennedy Juma, Jonas Mkude, Himid Mao, Feisal Salum Fei Toto, Shiza Kichuya, Yahya Zaydi, Thomas Ulimwengu, Rashid Mandawa, ShabaanIddi Chilunda

Hivi karibuni Kapombe alikwenda Afrika Kusini kufanyiwa uchunguzi wa jeraha alilopata wakati akiitumikia timu ya Taifa mwishoni mwa mwaka jana
Habari njema ni kwamba madaktari wameridhishwa na uponaji wa jeraha hilo hivyo kumruhusu Kapombe kuanza mazoezi mepesi
Kiraka huyo aliyekuwa nje ya dimba kwa takribani miezi mitano, anatarajiwa kuanza mazoezi mepesi wiki ijayo na huenda akarejea kikosini mapema kuwahi mchezo wa marudiano wa robo fainali ligi ya mabingwa dhidi ya TP Mazembe utakaopigwa April 12 au 13 huko DR Congo

Mchezo huo ambao ushindi ni lazima kwa Stars, utapigwa saa 12 jioni
Kocha Mkuu wa Stars Emmanuel Amunike amesema wamefanya maandalizi ya kutosha na anaamini vijana wake watafuata maelekezo na hatimaye kuibuka na ushindi
Ni mchezo ambao umeshikilia hatma ya Amunike kuendelea kuinoa Stars au kurejea kwao Nigeria kama atashindwa kuiongoza Stars kupata matokeo leo
Katika michezo iliyopita Amunike alikumbana na ukosoaji mkubwa kutoka kwa wadau wa soka nchini kutokana kutofurahishwa na uteuzi wa wachezaji, mbinu pamoja na upangaji wa kikosi chake
Stars ilikuwa na nafasi ya kufuzu mapema kama ingeweza kushinda mchezo uliopita dhidi ya Lesotho. Hata hivyo Amunike alipanga kikosi cha kujihami zaidi katika mchezo huo na kupelekea Stars kuchapwa bao 1-0 ugenini
Wengi wanasubiri kwa hamu kikosi atakachopanga leo dhidi ya Uganda ambapo Stars haihitaji matokeo mengine tofauti na ushindi
Lakini ni dhahiri hatma yake itakuwa mikononi mwake mwenyewe, kwani kama Stars haitashinda nae safari ya kurejea Nigeria itakuwa imewadia